< 2 Nyakati 18 >

1 Basi, Yehoshafati alikuwa na mali nyingi sana na heshima. Naye akafanya urafiki na Ahabu kwa mwanawe kumwoa binti wa Ahabu.
Josaphat avait des richesses et des honneurs en abondance, et il s'allia à Achab.
2 Baada ya miaka kadhaa akashuka kumtembelea Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja ngʼombe na kondoo wengi kwa ajili yake na watu aliokuwa amefuatana nao. Kisha Ahabu akamshawishi Yehoshafati kukwea pamoja naye ili kuishambulia Ramoth-Gileadi.
Après quelques années, il descendit auprès d'Achab à Samarie. Achab lui tua en abondance des moutons et des bovins, ainsi qu'au peuple qui était avec lui, et il le poussa à monter avec lui à Ramoth Galaad.
3 Ahabu mfalme wa Israeli akamuuliza Yehoshafati mfalme wa Yuda, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako. Tutakuwa pamoja nawe vitani.”
Achab, roi d'Israël, dit à Josaphat, roi de Juda: « Veux-tu aller avec moi à Ramoth Galaad? » Il lui répondit: « Je suis comme toi, et mon peuple comme ton peuple. Nous serons avec toi à la guerre. »
4 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
Josaphat dit au roi d'Israël: « Je te prie de t'enquérir d'abord de la parole de Yahvé. »
5 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda kwa kuwa Mungu ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
Alors le roi d'Israël rassembla les prophètes, quatre cents hommes, et leur dit: « Irai-je à Ramoth Galaad pour combattre, ou dois-je m'abstenir? » Ils ont dit: « Monte, car Dieu la livrera entre les mains du roi. »
6 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
Mais Josaphat dit: « N'y a-t-il pas ici un prophète de Yahvé en plus, pour que nous le consultions? »
7 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
Le roi d'Israël dit à Josaphat: « Il y a encore un homme par qui nous pouvons consulter Yahvé; mais je le déteste, car il ne prophétise jamais rien de bon à mon sujet, mais toujours du mal. C'est Michée, fils d'Imla. » Josaphat a dit: « Que le roi ne le dise pas. »
8 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
Alors le roi d'Israël appela un officier et dit: « Va vite chercher Michée, fils d'Imla. »
9 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
Le roi d'Israël et Josaphat, roi de Juda, étaient assis chacun sur son trône, revêtus de leurs robes, et ils étaient assis sur une place ouverte à l'entrée de la porte de Samarie; et tous les prophètes prophétisaient devant eux.
10 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
Sédécias, fils de Chenaana, se fit des cornes de fer et dit: « Yahvé dit: Avec celles-ci tu pousseras les Syriens jusqu'à ce qu'ils soient consumés. »
11 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho, wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
Tous les prophètes l'ont prophétisé, en disant: « Monte à Ramoth Galaad, et prospère, car Yahvé la livrera entre les mains du roi. »
12 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
Le messager qui était allé appeler Michée lui parla ainsi: « Voici, les paroles des prophètes disent du bien au roi d'une seule bouche. Que ta parole soit donc, je te prie, semblable à l'une des leurs, et qu'elle dise du bien. »
13 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
Michée dit: « L'Éternel est vivant, je dirai ce que mon Dieu dit. »
14 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa watatiwa mkononi mwako.”
Lorsqu'il fut arrivé auprès du roi, celui-ci lui dit: « Michée, irons-nous à Ramoth Galaad pour combattre, ou dois-je m'abstenir? » Il a dit: « Monte, et prospère. Ils seront livrés entre tes mains. »
15 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
Le roi lui dit: « Combien de fois t'adjurerai-je de ne me dire que la vérité au nom de Yahvé? »
16 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
Il dit: « J'ai vu tout Israël dispersé sur les montagnes, comme des brebis qui n'ont pas de berger. Yahvé a dit: « Elles n'ont pas de maître. Que chacun retourne en paix dans sa maison ».
17 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu bali mabaya tu?”
Le roi d'Israël dit à Josaphat: « Ne t'ai-je pas dit qu'il ne prophétiserait pas du bien à mon sujet, mais du mal? »
18 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama upande wa kulia na wa kushoto.
Michée dit: « C'est pourquoi écoutez la parole de l'Éternel. J'ai vu l'Éternel assis sur son trône, et toute l'armée des cieux debout à sa droite et à sa gauche.
19 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu, mfalme wa Israeli, ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
Yahvé dit: Qui séduira Achab, roi d'Israël, pour qu'il monte et tombe à Ramoth Galaad? L'un parlait en disant ceci, et l'autre en disant cela.
20 Mwishoni, roho akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’ “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’
Un esprit sortit, se tint devant l'Éternel, et dit: Je le séduirai. « Yahvé lui dit: « Comment?
21 “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
« Il a dit: « J'irai, et je serai un esprit de mensonge dans la bouche de tous ses prophètes ». « Il dit: 'Tu le séduiras, et tu l'emporteras aussi. Va et fais-le.
22 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
« Maintenant, voici que Yahvé a mis un esprit de mensonge dans la bouche de vos prophètes, et Yahvé a dit du mal de vous. »
23 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
Alors Sédécias, fils de Chenaana, s'approcha, frappa Michée sur la joue et dit: « Par où l'Esprit de Yahvé est-il sorti de moi pour te parler? »
24 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
Michée dit: « Voici ce que tu verras ce jour-là, quand tu entreras dans une pièce intérieure pour te cacher. »
25 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
Le roi d'Israël dit: « Prends Michée, et tu le porteras à Amon, gouverneur de la ville, et à Joas, fils du roi,
26 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
et tu diras: « Le roi dit: « Mets cet homme dans la prison, et nourris-le de pain d'affliction et d'eau d'affliction, jusqu'à ce que je revienne en paix »".
27 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
Michée dit: « Si vous revenez en paix, Yahvé n'a pas parlé par moi. » Il dit: « Écoutez, vous tous, peuple, tous! »
28 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
Le roi d'Israël et Josaphat, roi de Juda, montèrent à Ramoth Galaad.
29 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
Le roi d'Israël dit à Josaphat: « Je me déguiserai, et j'irai au combat; mais toi, mets tes vêtements. » Le roi d'Israël se déguisa donc, et ils allèrent au combat.
30 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
Or, le roi de Syrie avait donné cet ordre aux chefs de ses chars: « Ne combattez ni les petits ni les grands, si ce n'est seulement contre le roi d'Israël. »
31 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati, wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele, naye Bwana akamsaidia. Mungu akawaondoa kwake,
Lorsque les chefs des chars virent Josaphat, ils dirent: « C'est le roi d'Israël! » Ils firent donc demi-tour pour le combattre. Mais Josaphat cria, et l'Éternel le secourut, et Dieu les poussa à s'éloigner de lui.
32 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli nao wakaacha kumfuatilia.
Lorsque les chefs des chars virent que ce n'était pas le roi d'Israël, ils cessèrent de le poursuivre.
33 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma, mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
Un homme tira son arc au hasard et frappa le roi d'Israël entre les jointures de l'armure. Il dit alors au conducteur du char: « Fais demi-tour et emporte-moi hors de la bataille, car je suis gravement blessé. »
34 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye mfalme wa Israeli akajitegemeza ndani ya gari lake kuwaelekea Waaramu hadi jioni. Basi jioni yake akafa.
La bataille s'intensifia ce jour-là. Cependant, le roi d'Israël se soutint dans son char contre les Syriens jusqu'au soir; et vers le coucher du soleil, il mourut.

< 2 Nyakati 18 >