< 2 Nyakati 18 >

1 Basi, Yehoshafati alikuwa na mali nyingi sana na heshima. Naye akafanya urafiki na Ahabu kwa mwanawe kumwoa binti wa Ahabu.
Therfor Josaphat was riche and ful noble, and bi affynyte, `ethir alie, he was ioyned to Achab.
2 Baada ya miaka kadhaa akashuka kumtembelea Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja ngʼombe na kondoo wengi kwa ajili yake na watu aliokuwa amefuatana nao. Kisha Ahabu akamshawishi Yehoshafati kukwea pamoja naye ili kuishambulia Ramoth-Gileadi.
And aftir yeeris he cam doun to hym in to Samarie; at whos comyng Achab killide ful many wetheris and oxis, and to the puple that cam with hym; and he counseilide hym to stie in to Ramoth of Galaad.
3 Ahabu mfalme wa Israeli akamuuliza Yehoshafati mfalme wa Yuda, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako. Tutakuwa pamoja nawe vitani.”
And Achab, the kyng of Israel, seide to Josaphat, kyng of Juda, Come thou with me in to Ramoth of Galaad. To whom he answeride, As and Y am, thou art; as thi puple, so and my puple; and we schulen be with thee in batel.
4 Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
And Josaphat seide to the kyng of Israel, Y biseche, counsele thou in present tyme the word of the Lord.
5 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda kwa kuwa Mungu ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
Therfor the kyng of Israel gaderide togidere foure hundrid `men of prophetis, and seide to hem, Owen we to go in to Ramath of Galaad for to fiyte, ethir `take reste? And thei seiden, Stie ye, and God schal bitake in the hond of the king.
6 Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
And Josaphat seide, Whether no profete of the Lord is here, that we `axe also of hym?
7 Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
And the kyng of Israel seide to Josaphat, O man is, of whom we `moun axe the wille of the Lord, but and Y hate hym, for he prophecieth not good, but yuel to me in al tyme; sothely it is Mychee, the sone of Jebla. And Josaphat seide to hym, Kyng, speke thou not in this maner.
8 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
Therfor the kyng of Israel clepide oon of the geldyngis, and seide to hym, Clepe thou soone Mychee, the sone of Jebla.
9 Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
Forsothe the kyng of Israel and Josaphat, the kyng of Juda, saten euer eithir in his seete, and weren clothid in kyngis aray; forsothe thei saten in the cornfloor, `ether large hows, bisidis the yate of Samarie; and alle the prophetis profesieden bifor hem.
10 Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
Forsothe Sedechie, the sone of Cananee, made to hym yrone hornes, and seide, The Lord seith these thingis, With these thou schalt wyndewe Sirie, til thou al to-brake it.
11 Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho, wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
And alle prophetis profesieden in lijk maner, and seiden, Stie thou in to Ramoth of Galaad, and thou schalt haue prosperite; and the Lord schal bitake hem in to the hondis of the kyng.
12 Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
Forsothe the messanger, that yede to clepe Mychee, seide to hym, Lo! the wordis of alle prophetis tellen with o mouth goodis to the kyng; therfor, Y preye thee, that thi word disente not fro hem, and that thou speke prosperitees.
13 Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
To whom Mychee answeride, The Lord lyueth, for what euer thingis my Lord spekith to me, Y schal speke these thingis. Therfor he cam to the kyng.
14 Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa watatiwa mkononi mwako.”
To whom the kyng seide, Mychee, owen we go in to Ramoth of Galaad to fiyte, ether take reste? To whom he answeride, Stie ye, for alle prosperitees schulen come, and enemyes schulen be bitakun in to youre hondis.
15 Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
And the kyng seide, Eft and eft Y charge thee, that thou speke not to me no but that that is soth in the name of the Lord.
16 Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
And he seide, Y siy al Israel scaterid in the hillis, as scheep with out scheepherde. And the Lord seide, These men han not lordis; ech man turne ayen in to his hows in pees.
17 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu bali mabaya tu?”
The kyng of Israel seide to Josaphat, Whether Y seide not to thee, that he profesiede not ony good to me, but tho thingis that ben yuele?
18 Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama upande wa kulia na wa kushoto.
And therfor Mychee seide, Here ye the word of the Lord. Y siy the Lord sittynge in his trone, and al the oost of heuene stondynge nyy him at the riytside and `leftside.
19 Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu, mfalme wa Israeli, ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
And the Lord seide, Who schal disseyue Achab, the kyng of Israel, that he stie, and falle doun in Ramoth of Galaad? And whanne oon seide in this maner, and another seide in another maner, a spirit cam forth,
20 Mwishoni, roho akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’ “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’
and stood bifor the Lord, and seide, Y schal disseyue hym. To whom the Lord seide, `Wherynne, therfor schalt thou disseyue?
21 “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
And he answeride, Y schal go out, and Y schal be a `fals spirit in the mouth of alle hise profetis. And the Lord seide, Thou schalt disseyue, and thou schalt haue the maystri; go thou out, and do so.
22 “Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
Now therfor, lo! the Lord hath youe a spirit of leesyng in the mouth of alle thi prophetis, and the Lord spak yuels of thee.
23 Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
Forsothe Sedechie, the sone of Chananee, neiyide, and smoot `the cheke of Mychee, and seide, Bi what weye passide the Spirit of the Lord fro me to speke to thee?
24 Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
And Mychee seide, Thou thi silf schalt se in that dai, whanne thou schalt entre fro closet in to closet, that thou be hid.
25 Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
Sotheli the kyng of Israel comaundide, seiynge, Take ye Mychee, and lede ye hym to Amon, prince of the citee, and to Joas, the sone of Amalech;
26 Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
and ye schulen seie, The kyng seith these thingis, Sende ye this man in to prisoun, and yyue ye to hym a litil of breed, and a litil of watir, til Y turne ayen in pees.
27 Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
And Mychee seide, If thou turnest ayen in pees, the Lord spak not in me. And he seide, Alle `puplis here ye.
28 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
Therfor the kyng of Israel, and Josaphat, the kyng of Juda, stieden in to Ramoth of Galaad.
29 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
And the kyng of Israel seide to Josaphat, Y schal chaunge clothing, and so Y schal go to fiyte; but be thou clothid in thi clothis. Therfor whanne the kyng of Israel hadde chaungid clothing, he cam to batel.
30 Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
Forsothe the kyng of Sirie comaundide to the duykis of his multitude of knyytis, and seide, Fiyte ye not ayens the leeste, nether ayens the mooste; no but ayens the kyng aloone of Israel.
31 Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati, wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele, naye Bwana akamsaidia. Mungu akawaondoa kwake,
Therfor whanne the princes of the multitude of knyytis hadden seyn Josaphat, thei seiden, This is the kyng of Israel; and thei cumpassiden hym, and fouyten. And he criede to the Lord; and the Lord helpide hym, and turnede hem awey fro hym.
32 wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli nao wakaacha kumfuatilia.
Sotheli whanne the duykis of the multitude of knyytis hadden herd, that it was not the kyng of Israel, thei leften hym.
33 Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma, mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
Forsothe it bifelde, that oon of the puple schette an arewe in to vncerteyn, and smoot the kyng of Israel bitwixe the necke and the schuldris. And he seide to his charietere, Turne thin hond, and lede me out of the scheltrun; for Y am woundid.
34 Vita vikaendelea mchana kutwa, naye mfalme wa Israeli akajitegemeza ndani ya gari lake kuwaelekea Waaramu hadi jioni. Basi jioni yake akafa.
And the batel was endid in that dai. Certis the kyng of Israel stood in his chare ayens men of Sirye `til to euentid, and he diede, whanne the sunne yede doun.

< 2 Nyakati 18 >