< 2 Nyakati 17 >

1 Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
И воцарися Иосафат сын его вместо его, и укрепися Иосафат над Израилем:
2 Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
расположи же силу во всех градех Иудиных крепких и постави воеводы во градех Иудиных и во градех Ефремовых ихже побра прежде Аса отец его.
3 Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
И бысть Господь со Иосафатом, яко хождаше в путех Давида отца своего первых и не взыска идолов,
4 bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
но Господа Бога отца своего взыска и пойде в повелениих отца своего, а не по делом Израилевым:
5 Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
и укрепи Господь царство в руку его, и даша вся Иудеа дары Иосафату, и бысть ему богатство и слава многа.
6 Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
И вознесеся сердце его в пути Господни, и ктому изя высокая и дубравы от земли Иудины.
7 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
В третие же лето царства своего посла началники своя и сынов сильных Авдию и Захарию, и Нафанаила и Михеа, да учат во градех Иудиных:
8 Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
и с ними левити Самеа и Нафаниа, и Завдиа и Асиил, и Семирамоф и Ионафан, и Адониа и Товиа и Товадониа левити, и с ними Елисама и Иорам жерцы:
9 Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
учаху же во Иудеи, имеюще книгу закона Господня, и прохождаху грады Иудины и учаху люди.
10 Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
И бысть страх Господень на всех царствах земных окрест Иуды, и не воеваша противу Иосафата.
11 Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
И от иноплеменник Иосафату дары приношаху сребро и дани: Арави же привождаху ему овнов овчих седмь тысящ и седмь сот, и козлов седмь тысящ седмь сот.
12 Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
И бе Иосафат предуспевая велик в высоту и созда во Иудеи домы и грады крепки.
13 na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
И многа дела быша ему во Иудеи: и мужие ратницы крепцы сильнии во Иерусалиме.
14 Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
И сие число их по домом отечеств их: и во Иуде тысященачалницы Еднас вождь и с ним сынове сильнии силы триста тысящ:
15 aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
и по нем Иоанан началник и с ним двести осмьдесят тысящ:
16 aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
по немже Амасиа, сын Захариин, усердсвуяй Господу и с ним двести тысящ мужей сильных.
17 Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
И от Вениаминя сильнии силы Елиад, и с ним держащих лук и щиты двести тысящ сильных:
18 aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
и по нем Иозавад, и с ним сто осмьдесят тысящ, сильнии ко брани.
19 Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.
Сии служащии царю, кроме оных, ихже постави царь по градом крепким во всей Иудеи.

< 2 Nyakati 17 >