< 2 Nyakati 17 >
1 Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
Or Josaphat, son fils, régna en sa place, et prévalut contre Israël.
2 Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
Et il établit des légions de soldats dans toutes les villes de Juda qui étaient entourées de murs, et il posta des garnisons dans la terre de Juda et dans les villes d’Ephraïm qu’avait prises Asa, son père.
3 Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
Et le Seigneur fut avec Josaphat, parce qu’il marcha dans les premières voies de David, son père, et il n’espéra pas dans les Baalim,
4 bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
Mais dans le Dieu de son père; et il marcha dans ses préceptes, et non selon les péchés d’Israël.
5 Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
Et le Seigneur affermit le royaume en sa main, et tout Juda donna des présents à Josaphat; et il lui vint d’immenses richesses et beaucoup de gloire.
6 Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
Et, son cœur ayant pris de la hardiesse à cause des voies du Seigneur, il enleva de Juda même les hauts lieux et les bois sacrés.
7 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
Or, la troisième année de son règne, il envoya d’entre ses princes, Benhaïl, Obdias, Zacharie, Nathanaël et Michée, pour instruire dans les villes de Juda.
8 Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
Et avec eux les Lévites Séméias, Nathanias et Zabadias, Asaël, Sémiramoth et Jonathan, Adonias, Tobias et Thobadonias, et avec eux Elisama et Joran, prêtres.
9 Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
Et ils instruisaient le peuple en Juda, ayant le livre de la loi du Seigneur; ainsi ils parcouraient toutes les villes de Juda, et ils enseignaient le peuple.
10 Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
C’est pourquoi la crainte du Seigneur se répandit dans tous les royaumes des nations qui étaient aux environs de Juda, et ils n’osaient pas combattre contre Josaphat.
11 Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
Mais les Philistins même apportaient des présents à Josaphat, et un impôt d’argent: les Arabes aussi lui amenaient des troupeaux, sept mille sept cents béliers, et autant de boucs.
12 Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
Josaphat devint donc puissant, et s’éleva jusqu’à un très haut point de grandeur; et il bâtit dans Juda des maisons en forme de tour, et des villes murées.
13 na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
Et il prépara beaucoup d’ouvrages dans les villes de Juda; et il y avait aussi dans Jérusalem des hommes de guerre et vigoureux,
14 Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
Dont voici le nombre, selon les maisons et les familles de chacun: Dans Juda, les princes de l’armée étaient, Ednas, le chef, et avec lui étaient trois cent mille hommes très vigoureux.
15 aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
Après lui était Johanan, le prince, et avec lui deux cent quatre-vingt mille hommes;
16 aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
Après celui-ci, Amasias, fils de Zéchri, consacré au Seigneur, et avec lui deux cent mille hommes braves.
17 Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
À sa suite venait Eliada, vigoureux dans les combats, et avec lui deux cent mille hommes, tenant un arc et un bouclier.
18 aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
Après celui-ci était encore Jozabad, et avec lui cent quatre vingt mille soldats prêts à combattre,
19 Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.
Tous ceux-là étaient sous la main du roi, outre les autres qu’il avait placés dans les villes murées, dans tout Juda.