< 2 Nyakati 16 >
1 Katika mwaka wa thelathini na sita wa utawala wa Asa, Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
La trente-sixième année du règne d’Asa, Baasa, roi d’Israël, monta contre Juda, et il bâtit Rama, pour empêcher les gens d’Asa, roi de Juda, de sortir et d’entrer.
2 Ndipo Asa akachukua fedha na dhahabu kutoka hazina ya Hekalu la Bwana na kutoka jumba lake mwenyewe la kifalme na kumpelekea Ben-Hadadi mfalme wa Aramu, ambaye alikuwa anatawala huko Dameski.
Asa tira de l’argent et de l’or des trésors de la maison de Yahweh et de la maison du roi, et il envoya des messagers à Ben-Hadad, roi de Syrie, qui habitait à Damas, pour dire:
3 Akasema, “Pawepo na mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
« Qu’il y ait une alliance entre moi et toi, comme il y en avait une entre mon père et ton père. Je t’envoie de l’argent et de l’or. Va, romps ton alliance avec Baasa, roi d’Israël, afin qu’il s’éloigne de moi. »
4 Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Wakashinda Iyoni, Dani, Abel-Maimu na miji yote ya hazina ya Naftali.
Ben-Hadad écouta le roi Asa; il envoya les chefs de son armée contre les villes d’Israël, et ils battirent Ahion, Dan, Abel-Maïm et toutes les villes à magasins de Nephthali.
5 Baasha aliposikia jambo hili, akasimamisha kujenga Rama na kuacha kazi yake.
Baasa, l’ayant appris, cessa de bâtir Rama, et interrompit ses travaux.
6 Ndipo Mfalme Asa akawaleta watu wote wa Yuda, nao wakachukua mawe na miti ambayo Baasha alikuwa anavitumia huko Rama. Kwa vitu hivyo akajenga Geba na Mispa.
Le roi Asa prit tout Juda, et ils emportèrent les pierres et le bois avec lesquels Baasa construisait Rama; et il bâtit avec elles Gabaa et Maspha.
7 Ikawa wakati huo mwonaji Hanani akamjia Mfalme Asa wa Yuda na kumwambia: “Kwa sababu ulimtegemea mfalme wa Aramu nawe hukumtegemea Bwana Mungu wako, jeshi la mfalme wa Aramu limeponyoka mkononi mwako.
En ce temps-là, Hanani le voyant vint auprès d’Asa, roi de Juda, et lui dit: « Parce que tu t’es appuyé sur le roi de Syrie et que tu ne t’es pas appuyé sur Yahweh, ton Dieu, à cause de cela, l’armée du roi de Syrie s’est échappée de tes mains.
8 Je, hukumbuki lililotendeka kwa Wakushi na Walibia, hawakuwa jeshi lenye nguvu na magari mengi ya vita na wapanda farasi? Hata hivyo, ulipomtegemea Bwana yeye aliwatia mkononi mwako.
Les Éthiopiens et les Lybiens ne formaient-ils pas une grande armée, avec des chars, et des cavaliers très nombreux? Et cependant, parce que tu t’étais appuyé sur Yahweh, il les a livrés entre tes mains.
9 Kwa kuwa macho ya Bwana hukimbiakimbia duniani kote ili kujionyesha mwenye nguvu kwa ajili ya wale ambao mioyo yao inamtegemea kwa ukamilifu. Umefanya jambo la upumbavu na kuanzia sasa na kuendelea utakuwa na vita.”
Car les yeux de Yahweh parcourent toute la terre pour soutenir ceux dont le cœur est parfaitement à lui. Tu as donc agi en insensé dans cette affaire, car désormais tu auras des guerres. »
10 Asa akamkasirikia mwonaji kwa sababu ya jambo hili. Alikuwa ameghadhibika sana hata akamweka gerezani. Wakati huo huo Asa akaanza kuwatesa na kuwaonea baadhi ya watu kwa ukatili.
Asa fut irrité contre le voyant, et il le fit mettre en prison, car il était en colère contre lui à cause de ses paroles. Dans le même temps, Asa opprima quelques-uns du peuple.
11 Matukio ya utawala wa Asa, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
Et voici que les actes d’Asa, les premiers et les derniers, sont écrits dans le livre des rois de Juda et d’Israël.
12 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake, Asa alipatwa na ugonjwa kwenye miguu yake. Ingawa ugonjwa wake ulimzidia sana, hata katika kuugua kwake hakutafuta msaada kutoka kwa Bwana bali kwa matabibu tu.
Dans la trente-neuvième année de son règne, Asa eut les pieds malades au point d’éprouver de grandes souffrances; mais, même pendant sa maladie, il ne chercha pas Yahweh, mais les médecins.
13 Katika mwaka wa arobaini na moja wa utawala wa Asa, alikufa na kulala na baba zake.
Asa se coucha avec ses pères, et il mourut la quarante-unième année de son règne.
14 Nao wakamzika katika kaburi lile alilokuwa amejichongea mwenyewe katika Mji wa Daudi. Wakamzika kwa jeneza lililowekwa vikolezi na mchanganyiko wa manukato ya aina mbalimbali yaliyotengenezwa kwa utaalamu wa mtengeneza marashi, nao wakawasha moto mkubwa kwa heshima yake.
On l’enterra dans son sépulcre qu’il s’était creusé dans la ville de David; on le coucha sur un lit qu’on avait rempli de parfums et d’aromates préparés selon l’art du parfumeur, et l’on en brûla une quantité très considérable.