< 2 Nyakati 16 >

1 Katika mwaka wa thelathini na sita wa utawala wa Asa, Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
La trente-sixième année du règne d'Asa, Baescha, roi d'Israël, monta contre Juda et bâtit Rama, afin de ne permettre à personne de sortir ou d'entrer chez Asa, roi de Juda.
2 Ndipo Asa akachukua fedha na dhahabu kutoka hazina ya Hekalu la Bwana na kutoka jumba lake mwenyewe la kifalme na kumpelekea Ben-Hadadi mfalme wa Aramu, ambaye alikuwa anatawala huko Dameski.
Et Asa sortit de l'argent et de l'or des trésors de la maison de Yahvé et de la maison du roi, et il envoya à Ben Hadad, roi de Syrie, qui habitait à Damas, en disant:
3 Akasema, “Pawepo na mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
« Qu'il y ait un traité entre moi et toi, comme il y en a eu un entre mon père et ton père. Voici, je t'ai envoyé de l'argent et de l'or. Va, romps ton traité avec Baasha, roi d'Israël, afin qu'il s'éloigne de moi. »
4 Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Wakashinda Iyoni, Dani, Abel-Maimu na miji yote ya hazina ya Naftali.
Ben Hadad écouta le roi Asa et envoya les chefs de ses armées contre les villes d'Israël; ils frappèrent Ijon, Dan, Abel Maim et toutes les villes de stockage de Nephtali.
5 Baasha aliposikia jambo hili, akasimamisha kujenga Rama na kuacha kazi yake.
Lorsque Baasha l'apprit, il cessa de construire Rama et fit cesser ses travaux.
6 Ndipo Mfalme Asa akawaleta watu wote wa Yuda, nao wakachukua mawe na miti ambayo Baasha alikuwa anavitumia huko Rama. Kwa vitu hivyo akajenga Geba na Mispa.
Alors le roi Asa prit tout Juda, et on emporta les pierres et le bois de Rama, avec lesquels Baasha avait bâti, et il bâtit avec eux Guéba et Mitspa.
7 Ikawa wakati huo mwonaji Hanani akamjia Mfalme Asa wa Yuda na kumwambia: “Kwa sababu ulimtegemea mfalme wa Aramu nawe hukumtegemea Bwana Mungu wako, jeshi la mfalme wa Aramu limeponyoka mkononi mwako.
En ce temps-là, Hanani le devin vint auprès d'Asa, roi de Juda, et lui dit: « Parce que tu t'es appuyé sur le roi de Syrie et que tu n'as pas compté sur Yahvé ton Dieu, l'armée du roi de Syrie s'est échappée de tes mains.
8 Je, hukumbuki lililotendeka kwa Wakushi na Walibia, hawakuwa jeshi lenye nguvu na magari mengi ya vita na wapanda farasi? Hata hivyo, ulipomtegemea Bwana yeye aliwatia mkononi mwako.
Les Éthiopiens et les Lubim n'étaient-ils pas une grande armée, avec des chars et un très grand nombre de cavaliers? Mais, parce que tu t'es appuyé sur Yahvé, il les a livrés entre tes mains.
9 Kwa kuwa macho ya Bwana hukimbiakimbia duniani kote ili kujionyesha mwenye nguvu kwa ajili ya wale ambao mioyo yao inamtegemea kwa ukamilifu. Umefanya jambo la upumbavu na kuanzia sasa na kuendelea utakuwa na vita.”
Car les yeux de Yahvé vont et viennent sur toute la terre, pour se montrer fort en faveur de ceux dont le cœur est parfait envers lui. Vous avez fait une folie en cela, car désormais vous aurez des guerres. »
10 Asa akamkasirikia mwonaji kwa sababu ya jambo hili. Alikuwa ameghadhibika sana hata akamweka gerezani. Wakati huo huo Asa akaanza kuwatesa na kuwaonea baadhi ya watu kwa ukatili.
Alors Asa s'irrita contre le devin, et le mit en prison, car il était furieux contre lui à cause de cette chose. En même temps, Asa opprima une partie du peuple.
11 Matukio ya utawala wa Asa, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
Voici les actes d'Asa, les premiers et les derniers, ils sont écrits dans le livre des rois de Juda et d'Israël.
12 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake, Asa alipatwa na ugonjwa kwenye miguu yake. Ingawa ugonjwa wake ulimzidia sana, hata katika kuugua kwake hakutafuta msaada kutoka kwa Bwana bali kwa matabibu tu.
La trente-neuvième année de son règne, Asa fut atteint d'une maladie des pieds. Sa maladie était extrêmement grave; cependant, dans sa maladie, il ne chercha pas Yahvé, mais seulement les médecins.
13 Katika mwaka wa arobaini na moja wa utawala wa Asa, alikufa na kulala na baba zake.
Asa se coucha avec ses pères et mourut la quarante et unième année de son règne.
14 Nao wakamzika katika kaburi lile alilokuwa amejichongea mwenyewe katika Mji wa Daudi. Wakamzika kwa jeneza lililowekwa vikolezi na mchanganyiko wa manukato ya aina mbalimbali yaliyotengenezwa kwa utaalamu wa mtengeneza marashi, nao wakawasha moto mkubwa kwa heshima yake.
On l'enterra dans son propre tombeau, qu'il s'était creusé dans la ville de David, et on le coucha dans le lit qui était rempli d'aromates et de diverses sortes d'épices préparées par l'art des parfumeurs; et on fit pour lui un très grand feu.

< 2 Nyakati 16 >