< 2 Nyakati 16 >

1 Katika mwaka wa thelathini na sita wa utawala wa Asa, Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
我我我阿撒當國第三十六年,以色列王巴厄沙來進攻猶大,在辣瑪修築工事,防止人同猶大王阿撒來往。
2 Ndipo Asa akachukua fedha na dhahabu kutoka hazina ya Hekalu la Bwana na kutoka jumba lake mwenyewe la kifalme na kumpelekea Ben-Hadadi mfalme wa Aramu, ambaye alikuwa anatawala huko Dameski.
當時阿撒拿出上主殿內和王宮府庫中的金銀,送給住在大馬士革得阿蘭王本哈達得說:
3 Akasema, “Pawepo na mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
「我與你之間,以及我父與你之間都立過約;現在我給你送來金銀作為禮品,請你廢除你與以色列王巴厄沙所立的約,使他離開我的國境。」
4 Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Wakashinda Iyoni, Dani, Abel-Maimu na miji yote ya hazina ya Naftali.
本哈達得聽從了阿撒王的話,即刻派軍長,去攻打以色列的城市,攻下了依雍、丹、阿貝耳瑪因和納斐塔里所有的屯貨城。
5 Baasha aliposikia jambo hili, akasimamisha kujenga Rama na kuacha kazi yake.
巴厄沙一聽說這事,立即停止在辣瑪的工事。
6 Ndipo Mfalme Asa akawaleta watu wote wa Yuda, nao wakachukua mawe na miti ambayo Baasha alikuwa anavitumia huko Rama. Kwa vitu hivyo akajenga Geba na Mispa.
阿撒王遂徵調全猶大人,將巴厄沙修築辣瑪所用的石頭和木材運走,用來修築革巴和米茲帕。[先見者哈納尼的斥責]
7 Ikawa wakati huo mwonaji Hanani akamjia Mfalme Asa wa Yuda na kumwambia: “Kwa sababu ulimtegemea mfalme wa Aramu nawe hukumtegemea Bwana Mungu wako, jeshi la mfalme wa Aramu limeponyoka mkononi mwako.
那時,先見者哈納尼來見猶大王阿撒,對他說:「因為你依靠了阿蘭,而沒有依靠上主你的天主,因此阿蘭王的軍隊脫離了你。
8 Je, hukumbuki lililotendeka kwa Wakushi na Walibia, hawakuwa jeshi lenye nguvu na magari mengi ya vita na wapanda farasi? Hata hivyo, ulipomtegemea Bwana yeye aliwatia mkononi mwako.
雇士人和利比亞人不是一支很強大的軍隊嗎﹖戰車騎兵不是很多嗎﹖但幾時你依靠上主,他便將他們交在你的手中。
9 Kwa kuwa macho ya Bwana hukimbiakimbia duniani kote ili kujionyesha mwenye nguvu kwa ajili ya wale ambao mioyo yao inamtegemea kwa ukamilifu. Umefanya jambo la upumbavu na kuanzia sasa na kuendelea utakuwa na vita.”
上主的眼遍察各地,對所有專心忠於他的,他必大顯威能,加以扶助。你這事作得太無知了,今後你必要遭遇戰禍。」
10 Asa akamkasirikia mwonaji kwa sababu ya jambo hili. Alikuwa ameghadhibika sana hata akamweka gerezani. Wakati huo huo Asa akaanza kuwatesa na kuwaonea baadhi ya watu kwa ukatili.
阿撒對先見者發怒,將他囚在獄中;王在這事上實在生了大氣,同時阿撒又虐待了一些百姓。[阿撒逝世 ]
11 Matukio ya utawala wa Asa, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
阿撒的前後事蹟,都記載在猶大和以色列列王實錄上。
12 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake, Asa alipatwa na ugonjwa kwenye miguu yake. Ingawa ugonjwa wake ulimzidia sana, hata katika kuugua kwake hakutafuta msaada kutoka kwa Bwana bali kwa matabibu tu.
阿撒當國第三十九年,患了足疾,病得十分嚴重;他在病中不求上主,而只求醫。
13 Katika mwaka wa arobaini na moja wa utawala wa Asa, alikufa na kulala na baba zake.
阿撒在位四十一年逝世,與祖先同眠。
14 Nao wakamzika katika kaburi lile alilokuwa amejichongea mwenyewe katika Mji wa Daudi. Wakamzika kwa jeneza lililowekwa vikolezi na mchanganyiko wa manukato ya aina mbalimbali yaliyotengenezwa kwa utaalamu wa mtengeneza marashi, nao wakawasha moto mkubwa kwa heshima yake.
人們將他葬在達味城,自己所鑿的墳墓,將他放在床上面,滿堆香料,即照調香法所製的各種香料,又為他焚燒了很多的香料。

< 2 Nyakati 16 >