< 2 Nyakati 16 >

1 Katika mwaka wa thelathini na sita wa utawala wa Asa, Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
В тридесет и шестата година от царуването на Аса, Израилевият цар Вааса, като възлезе против Юда, съгради Рама, за да не остави никого да излиза от Юдовия цар Аса, нито да влиза при него.
2 Ndipo Asa akachukua fedha na dhahabu kutoka hazina ya Hekalu la Bwana na kutoka jumba lake mwenyewe la kifalme na kumpelekea Ben-Hadadi mfalme wa Aramu, ambaye alikuwa anatawala huko Dameski.
Тогава Аса извади сребро и злато из съкровищницата на Господния дом и на царската къща та прати при сирийския цар Венадад, който жевееше в Дамаск, да рекат:
3 Akasema, “Pawepo na mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
Нека има договар между мене и тебе, както е имало между баща ми и твоя баща; ето пратих ти сребро и злато; иди, развали договора си с Израилевия цар Вааса, за да се оттегли от мене.
4 Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Wakashinda Iyoni, Dani, Abel-Maimu na miji yote ya hazina ya Naftali.
И Венадад послуша цар Аса та прати началниците на силите си против Израилевите градове; и те поразиха Иион, Дан, Авел-маим и всичките Нефталимови житници-градове.
5 Baasha aliposikia jambo hili, akasimamisha kujenga Rama na kuacha kazi yake.
И Вааса, като чу това, престана да гради Рама, и преустанови работата си.
6 Ndipo Mfalme Asa akawaleta watu wote wa Yuda, nao wakachukua mawe na miti ambayo Baasha alikuwa anavitumia huko Rama. Kwa vitu hivyo akajenga Geba na Mispa.
Тогава цар Аса взе целия Юда, та дигнаха камъните на Рама и дърветата й, с които Вааса градеше; и с тях съгради Гава и Масфа.
7 Ikawa wakati huo mwonaji Hanani akamjia Mfalme Asa wa Yuda na kumwambia: “Kwa sababu ulimtegemea mfalme wa Aramu nawe hukumtegemea Bwana Mungu wako, jeshi la mfalme wa Aramu limeponyoka mkononi mwako.
А в това време гледачът Ананий отиде при Юдовия цар Аса та му рече: Понеже си уповал на сирийския цар, а не си уповавал на Господа своя Бог, затова войската на сирийския цар избегна и ръката ти.
8 Je, hukumbuki lililotendeka kwa Wakushi na Walibia, hawakuwa jeshi lenye nguvu na magari mengi ya vita na wapanda farasi? Hata hivyo, ulipomtegemea Bwana yeye aliwatia mkononi mwako.
Етоипяните и ливийците не бяха ли огромно множество, с твърде много колесници и конници? Но пак, понеже ти упова на Господа, Той ги предаде в ръката ти.
9 Kwa kuwa macho ya Bwana hukimbiakimbia duniani kote ili kujionyesha mwenye nguvu kwa ajili ya wale ambao mioyo yao inamtegemea kwa ukamilifu. Umefanya jambo la upumbavu na kuanzia sasa na kuendelea utakuwa na vita.”
Защото очите на Господа се обръщат насам-натам през целия свят, за да се показва Той мощен в помощ на ония, чиито сърца са съвършенно разположени към Него. В това ти си постъпил безумно, защото от сега нататък ще имаш войни.
10 Asa akamkasirikia mwonaji kwa sababu ya jambo hili. Alikuwa ameghadhibika sana hata akamweka gerezani. Wakati huo huo Asa akaanza kuwatesa na kuwaonea baadhi ya watu kwa ukatili.
По това, Аса се разгневи на гледача та го тури в затвор, защото се разсърди против него за туй нещо. И в същото време Аса притесни някои от людете.
11 Matukio ya utawala wa Asa, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
И, ето, делата на Аса, първите и последните, ето, написани са в Книгата на Юдовите и Израилевите царе.
12 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake, Asa alipatwa na ugonjwa kwenye miguu yake. Ingawa ugonjwa wake ulimzidia sana, hata katika kuugua kwake hakutafuta msaada kutoka kwa Bwana bali kwa matabibu tu.
А в тридесет и деветата година от царуването си, Аса се разболя от болест в нозете; обаче, макар болестта му да ставаше твърде тежка, пак в болестта си той не потърси Господа, но лекарите.
13 Katika mwaka wa arobaini na moja wa utawala wa Asa, alikufa na kulala na baba zake.
И Аса заспа с бащите си; и умря в четиридесет и първата година от царуването си.
14 Nao wakamzika katika kaburi lile alilokuwa amejichongea mwenyewe katika Mji wa Daudi. Wakamzika kwa jeneza lililowekwa vikolezi na mchanganyiko wa manukato ya aina mbalimbali yaliyotengenezwa kwa utaalamu wa mtengeneza marashi, nao wakawasha moto mkubwa kwa heshima yake.
И погребаха го в гроба, който се бе изкопал в Давидовия град, и положиха го на легло пълно с благоухания и с различни аптекарски аромати; и изгориха за него твърде много аромати.

< 2 Nyakati 16 >