< 2 Nyakati 15 >

1 Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi.
Wtedy Duch Boży zstąpił na Azariasza, syna Obeda.
2 Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi.
I wyszedł on naprzeciw Asy, i powiedział mu: Słuchajcie mnie, Aso i całe [pokolenie] Judy i Beniamina. PAN [jest] z wami, dopóki jesteście z nim. Jeśli go szukać będziecie, znajdziecie go, ale jeśli go opuścicie, on opuści was.
3 Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria.
Przez wiele dni Izrael był bez prawdziwego Boga, bez nauczającego kapłana i bez prawa.
4 Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao.
Gdy jednak w swoim nieszczęściu nawrócili się do PANA, Boga Izraela, i szukali go, dawał się im odnaleźć.
5 Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa.
W tamtych czasach nie było pokoju ani dla wychodzącego, ani dla wchodzącego, gdyż wielkie udręki spotkały wszystkich mieszkańców ziemi.
6 Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina.
I naród występował przeciw narodowi, a miasto – przeciw miastu, ponieważ Bóg ich zatrważał wszelkim nieszczęściem.
7 Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”
Wy więc umacniajcie się i niech nie słabną wasze ręce, bo czeka [was] zapłata za waszą pracę.
8 Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.
A gdy Asa usłyszał te słowa i proroctwo proroka Obeda, umocnił się i usunął obrzydliwości z całej ziemi Judy i Beniamina, a także z miast, które zdobył na górze Efraim, i odnowił ołtarz PANA, który [stał] przed przedsionkiem PANA.
9 Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
Potem zebrał cały [lud z] Judy i Beniamina oraz przybyszów, [którzy byli] z nimi z Efraima, Manassesa i Symeona. Bardzo wielu bowiem zbiegło z Izraela do niego, widząc, że z nim był PAN, jego Bóg.
10 Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
Zgromadzili się więc w Jerozolimie w trzecim miesiącu, w piętnastym roku panowania Asy.
11 Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka.
W tym dniu złożyli PANU ofiary z łupów, [które] przynieśli: siedemset wołów i siedem tysięcy owiec.
12 Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote.
I zobowiązali się przymierzem szukać PANA, Boga swoich ojców, z całego swego serca i całą swoją duszą;
13 Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke.
I że ktokolwiek nie będzie szukał PANA, Boga Izraela, poniesie śmierć – czy to mały, czy wielki, mężczyzna czy kobieta.
14 Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu.
I przysięgli PANU donośnym głosem, wśród okrzyków oraz [dźwięków] trąb i kornetów.
15 Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.
A cały lud Judy radował się z tej przysięgi, ponieważ przysięgli z całego serca i z całą chęcią szukali go, a dał się im odnaleźć. I dał im PAN odpoczynek ze wszystkich stron.
16 Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
Ponadto nawet [swoją] matkę Maakę król Asa pozbawił godności królowej, ponieważ sporządziła posąg w gaju. I Asa ściął jej posąg, pokruszył go i spalił przy potoku Cedron.
17 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
A choć wyżyny nie zostały zniesione z Izraela, to jednak serce Asy było doskonałe przez wszystkie jego dni.
18 Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Sprowadził też do domu Bożego to, co poświęcił jego ojciec i co on [sam] poświęcił: srebro, złoto i naczynia.
19 Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.
I nie było wojny aż do trzydziestego piątego roku panowania Asy.

< 2 Nyakati 15 >