< 2 Nyakati 15 >

1 Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi.
Immay ti espiritu ti Dios kenni Azarias a putot ni Obed.
2 Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi.
Napanna sinabat ni Asa ket kinunana kenkuana, “Dumngegka kaniak Asa, ken dagiti amin a tattao ti Juda ken Benjamin: Adda kadakayo ni Yahweh, kabayatan iti kaaddayo kenkuana. No sapulenyo isuna, masarakanyonto isuna; ngem no tallikudanyo isuna, baybay-annakayonto.
3 Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria.
Ita, nabayag a tiempo nga awan iti Israel ti pudno a Dios, ken awan padi a mangisuro, ken awan linteg.
4 Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao.
Ngem iti tiempo ti pannakaparigatda, nagsublida kenni Yahweh a Dios ti Israel, sinapulda isuna, ket nasarakanda.
5 Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa.
Kadagidiay a tiempo, awan talna iti tao nga agdaliasat iti sadinoman; ngem ketdi, adda nakaro a pannakariribuk kadagiti amin nga agnanaed kadagiti daga.
6 Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina.
Narumekrumekda, nasion maibusor iti nasion, ken siudad maibusor iti siudad, ta riniribuk ida ti Dios babaen kadagiti amin a kita ti panagsagaba.
7 Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”
Ngem bumilegkayo koma, ket saanyo nga ipalubos a kumapsut dagiti imayo, ta magunggonaanto ti trabahoyo.”
8 Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.
Idi nangngeg ni Asa dagitoy a sasao, a padto ni profeta Obed, timmured isuna ket inikkatna dagiti makarimon a banbanag iti amin a daga ti Juda ken Benjamin ken kadagiti siudad a sinakupna iti katurturodan a pagilian ti Efraim; ken tinarimaanna ti altar ni Yahweh nga adda iti sangoanan ti balkon ti balay ni Yahweh.
9 Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
Inummongna dagiti amin a tattao iti Juda ken Benjamin, ken dagiti makipagnanaed kadakuada-dagiti tattao a nagtaud iti Efraim, Manases ken Simeon. Ta aduda a naggapu iti Israel a napan kenkuana, idi nakitada nga adda kenkuana ni Yahweh a Diosna.
10 Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
Isu a naguummongda idiay Jerusalem iti maikatlo a bulan, iti maika-sangapulo ket lima a tawen a panagturay ni Asa.
11 Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka.
Iti dayta nga aldaw, indatonda kenni Yahweh ti dadduma a sinamsamda nga awitda; pito gasut a bulog a baka ken pito ribu a karnero ken kalding.
12 Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote.
Nagaramidda iti katulagan a sapulenda ni Yahweh a Dios dagiti kapuonanda, iti amin a pusoda ken iti amin a kararuada.
13 Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke.
Immanamongda a siasinoman a saan a mangsapul kenni Yahweh a Dios ti Israel ket rumbeng a mapapatay, ubing man wenno nataengan, lalaki man wenno babai.
14 Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu.
Nagsapatada kenni Yahweh iti napigsa a timek, babaen iti panagpukpukkawda, ken babaen kadagiti trumpeta ken tangguyob.
15 Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.
Nagrag-o dagiti amin a tattao ti Juda gapu iti sapata, ta nagsapatada iti amin a pusoda, ken sinapulda ni Yahweh iti amin a tarigagayda; ket nasarakanda isuna. Inikkan ida ni Yahweh iti talna iti aglawlawda.
16 Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
Inikkatna pay ni Maaca, nga apongna a babai manipud iti kinareynana, gapu ta nagaramid isuna iti makarimon nga imahen ni Asera. Tinumba ni Asa ti makarimon nga imahen, binurakna sana pinuoran daytoy idiay waig ti Kidron.
17 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
Ngem saan a naikkat dagiti pagdaydayawan idiay Israel. Nupay kasta, naan-anay a napudno ti puso ni Asa kadagiti amin nga aldawna.
18 Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Impanna iti balay ti Dios dagiti alikamen ti amana ken dagiti bukodna nga alikamen a kukua ni Yahweh: dagiti pirak ken balitok.
19 Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.
Awanen ti gubat agingga iti maika-35 a tawen a panagturay ni Asa.

< 2 Nyakati 15 >