< 2 Nyakati 15 >

1 Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi.
and Azariah son: child Oded to be upon him spirit God
2 Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi.
and to come out: come to/for face: before Asa and to say to/for him to hear: hear me Asa and all Judah and Benjamin LORD with you in/on/with to be you with him and if to seek him to find to/for you and if to leave: forsake him to leave: forsake [obj] you
3 Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria.
and day many to/for Israel to/for not God truth: true and to/for not priest to show and to/for not instruction
4 Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao.
and to return: turn back in/on/with distress to/for him upon LORD God Israel and to seek him and to find to/for them
5 Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa.
and in/on/with time [the] they(masc.) nothing peace to/for to come out: come and to/for to come (in): come for tumult many upon all to dwell [the] land: country/planet
6 Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina.
and to crush nation in/on/with nation and city in/on/with city for God to confuse them in/on/with all distress
7 Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”
and you(m. p.) to strengthen: strengthen and not to slacken hand your for there wages to/for wages your
8 Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.
and like/as to hear: hear Asa [the] word [the] these and [the] prophecy (Azariah son: child *X*) Oded [the] prophet to strengthen: strengthen and to pass: bring [the] abomination from all land: country/planet Judah and Benjamin and from [the] city which to capture from mountain: hill country Ephraim and to renew [obj] altar LORD which to/for face: before Portico LORD
9 Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
and to gather [obj] all Judah and Benjamin and [the] to sojourn with them from Ephraim and Manasseh and from Simeon for to fall: deserting upon him from Israel to/for abundance in/on/with to see: see they for LORD God his with him
10 Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
and to gather Jerusalem in/on/with month [the] third to/for year five ten to/for royalty Asa
11 Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka.
and to sacrifice to/for LORD in/on/with day [the] he/she/it from [the] spoil to come (in): bring cattle seven hundred and flock seven thousand
12 Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote.
and to come (in): come in/on/with covenant to/for to seek [obj] LORD God father their in/on/with all heart their and in/on/with all soul their
13 Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke.
and all which not to seek to/for LORD God Israel to die to/for from small: young and till great: large to/for from man and till woman
14 Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu.
and to swear to/for LORD in/on/with voice great: large and in/on/with shout and in/on/with trumpet and in/on/with trumpet
15 Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.
and to rejoice all Judah upon [the] oath for in/on/with all heart their to swear and in/on/with all acceptance their to seek him and to find to/for them and to rest LORD to/for them from around
16 Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
and also Maacah mother Asa [the] king to turn aside: remove her from queen which to make to/for Asherah horror and to cut: cut Asa [obj] horror her and to crush and to burn in/on/with torrent: valley Kidron
17 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
and [the] high place not to turn aside: remove from Israel except heart Asa to be complete all day his
18 Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
and to come (in): bring [obj] holiness father his and holiness his house: temple [the] God silver: money and gold and article/utensil
19 Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.
and battle not to be till year thirty and five to/for royalty Asa

< 2 Nyakati 15 >