< 2 Nyakati 15 >

1 Roho wa Bwana akamjia Azaria mwana wa Odedi.
Then the Spirite of God came vpon Azariah the sonne of Obed.
2 Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini. Bwana yu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi.
And he went out to meete Asa, and said vnto him, O Asa, and all Iudah, and Beniamin, heare ye me. The Lord is with you, while ye be with him: and if ye seeke him, he wil be founde of you, but if ye forsake him, he will forsake you.
3 Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha na wala hawakuwa na sheria.
Nowe for a long season Israel hath bene without the true God, and without Priest to teach and without Lawe.
4 Lakini katika taabu yao walimrudia Bwana, Mungu wa Israeli na kumtafuta, naye akaonekana kwao.
But whosoeuer returned in his affliction to the Lord God of Israel, and sought him, he was founde of them.
5 Katika siku hizo hapakuwa na amani kwa yeyote aliyesafiri, kutoka wala kuingia, kwa kuwa wakazi wote wa nchi walikuwa katika machafuko makubwa.
And in that time there was no peace to him, that did goe out and goe in: but great troubles were to all the inhabitants of the earth.
6 Taifa moja lilipigana na taifa lingine na mji mmoja ukapigana na mji mwingine, kwa sababu Mungu alikuwa anawahangaisha kwa taabu za kila aina.
For nation was destroyed of nation, and citie of citie: for God troubled them with all aduersitie.
7 Lakini kwa habari yenu ninyi, kuweni hodari wala msikate tamaa, kwa kuwa mtapata thawabu kwa kazi yenu.”
Be ye strong therefore, and let not your handes be weake: for your worke shall haue a rewarde.
8 Asa aliposikia maneno haya na unabii wa Azaria mwana wa Odedi nabii, akajipa moyo. Akaziondoa sanamu zote zilizokuwa machukizo katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na kutoka miji aliyoiteka ya vilima vya Efraimu. Akakarabati madhabahu ya Bwana iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Hekalu la Bwana.
And when Asa heard these wordes, and the prophesie of Obed the Prophet, he was encouraged, and tooke away the abominations out of all the lande of Iudah, and Beniamin, and out of the cities which he had taken of mount Ephraim, and he renued the altar of the Lord, that was before the porche of the Lord.
9 Kisha akakutanisha Yuda wote, Benyamini na watu kutoka Efraimu, watu wa Manase na Simeoni waliokuwa wanaishi miongoni mwao, kwa maana idadi kubwa walikuwa wamemjia kutoka Israeli walipoona kwamba Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
And he gathered all Iudah and Beniamin, and the strangers with them out of Ephraim, and Manasseh, and out of Simeon: for there fell many to him out of Israel, when they sawe that the Lord his God was with him.
10 Basi wakakusanyika huko Yerusalemu mwezi wa tatu katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
So they assembled to Ierusalem in the third moneth, in the fifteenth yere of the reigne of Asa.
11 Wakati huo wakamtolea Bwana dhabihu za ngʼombe 700, kondoo na mbuzi 7,000 kutoka zile nyara walizoteka.
And they offred vnto the Lord the same time of the spoyle, which they had brought, euen seuen hundreth bullockes, and seuen thousande sheepe.
12 Wakafanya agano kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote.
And they made a couenant to seeke the Lord God of their fathers, with all their heart, and with all their soule.
13 Wale wote ambao hawangemtafuta Bwana, Mungu wa Israeli wangelazimika kuuawa, akiwa mdogo au mkubwa, mwanaume au mwanamke.
And whosoeuer will not seeke the Lord God of Israel, shalbe slaine, whether he were small or great, man or woman.
14 Wakamwapia Bwana kwa sauti kuu, kwa kupiga kelele, tarumbeta na kwa mabaragumu.
And they sware vnto the Lord with a loude voyce, and with shouting and with trumpets, and with cornets.
15 Yuda wote wakafurahia kile kiapo kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wao wote. Wakamtafuta Mungu kwa bidii, naye akaonekana kwao. Kwa hiyo Bwana akawastarehesha pande zote.
And all Iudah reioyced at the othe: for they had sworne vnto the Lord with all their heart, and sought him with a whole desire, and he was founde of them. And the Lord gaue them rest rounde about.
16 Mfalme Asa akamwondolea Maaka mama yake wadhifa wake kama mama malkia kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo, akaivunjavunja na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
And King Asa deposed Maachah his mother from her regencie, because she had made an idole in a groue: and Asa brake downe her idole, and stamped it, and burnt it at the brooke Kidron.
17 Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika Israeli, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
But the hie places were not taken away out of Israel: yet the heart of Asa was perfit all his dayes.
18 Akaleta ndani ya Hekalu la Mungu fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
Also he brought into the house of God the things that his father had dedicate, and that he had dedicate, siluer, and golde, and vessels.
19 Hapakuwepo vita tena mpaka mwaka wa thelathini na tano wa utawala wake Asa.
And there was no warre vnto the fiue and thirtieth yeere of the reigne of Asa.

< 2 Nyakati 15 >