< 2 Nyakati 14 >

1 Naye Abiya akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi.
E Abias dormiu com seus pais e o sepultaram na cidade de David; e Asa, seu filho, reinou em seu lugar: nos seus dias esteve a terra em paz dez anos.
2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Bwana Mungu wake.
E Asa fez o que era bom e reto aos olhos do Senhor seu Deus.
3 Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, akayavunja yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Maashera.
Porque tirou os altares dos deuses estranhos, e os altos: e quebrou as estátuas, e cortou os bosques.
4 Akawaamuru Yuda kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao na kutii sheria zake na amri zake.
E mandou a Judá que buscassem ao Senhor Deus de seus pais, e que observassem a lei e o mandamento.
5 Akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu za kufukizia uvumba kwenye kila mji katika Yuda, nao ufalme ulikuwa na amani katika utawala wake.
Também tirou de todas as cidades de Judá os altos e as imagens do sol: e o reino esteve quieto diante dele.
6 Akajenga miji yenye ngome katika Yuda, wakati nchi ikiwa na amani. Hakuna mtu yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa kuwa Bwana alimstarehesha.
E edificou cidades fortes em Judá: porque a terra estava quieta, e não havia guerra contra ele naqueles anos; porquanto o Senhor lhe dera repouso.
7 Mfalme akawaambia Yuda, “Tuijenge hii miji na tuizungushie kuta, pamoja na minara, malango na makomeo. Nchi bado ni yetu, kwa sababu tumemtafuta Bwana Mungu wetu, tulimtafuta naye ametupa raha kila upande.” Hivyo wakajenga na wakafanikiwa.
Disse pois a Judá: Edifiquemos estas cidades, e cerquemo-las de muros e torres, portas e ferrolhos, enquanto a terra ainda está quieta diante de nós, pois buscamos ao Senhor nosso Deus; buscamo-lo, e deu-nos repouso em redor. Edificaram, pois, e prosperaram.
8 Asa alikuwa na jeshi la watu 300,000 kutoka Yuda, wenye ngao kubwa na mikuki na jeshi la watu 280,000 kutoka Benyamini, wenye ngao ndogo na pinde. Watu hawa wote walikuwa wapiganaji mashujaa.
Tinha pois Asa um exército de trezentos mil de Judá que traziam pavez e lança; e duzentos e oitenta mil de Benjamin, que traziam escudo e atiravam de arco; todos estes eram varões valentes.
9 Zera Mkushi akatoka kupigana dhidi yao akiwa na jeshi la watu maelfu ya maelfu na magari ya vita 300, nao wakaja mpaka Maresha.
E Zera, o ethiope, saiu contra eles, com um exército de mil milhares, e trezentos carros, e chegou até Maresa.
10 Asa akatoka kumkabili, nao wakapanga vita katika Bonde la Sefatha karibu na Maresha.
Então Asa saiu contra ele: e ordenaram a batalha no vale de Zephatha, junto a Maresa.
11 Kisha Asa akamlilia Bwana Mungu wake na kusema, “Ee Bwana, hakuna yeyote aliye kama wewe wa kuwasaidia wasio na nguvu dhidi ya wenye nguvu. Utusaidie, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, kwa kuwa tunakutumainia wewe, nasi kwa jina lako tumekuja dhidi ya jeshi hili kubwa. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, usiwaache wanadamu wakushinde wewe.”
E Asa clamou ao Senhor seu Deus, e disse: Senhor, nada para ti é ajudar, quer o poderoso quer o de nenhuma força; ajuda-nos, pois, Senhor nosso Deus, porque em ti confiamos, e no teu nome viemos contra esta multidão: Senhor, tu és nosso Deus, não prevaleça contra ti o homem
12 Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa na Yuda. Wakushi wakakimbia,
E o Senhor feriu os ethiopes diante d'Asa e diante de Judá: e fugiram os ethiopes.
13 naye Asa na jeshi lake wakawafuatia mpaka Gerari. Idadi kubwa ya Wakushi ilianguka hata wasiweze kuinuka tena, wakapondapondwa mbele za Bwana na majeshi yake.
E Asa, e o povo que estava com ele os perseguiram até Gerar, e cairam tantos dos ethiopes, que já não havia neles vigor algum; porque foram quebrantados diante do Senhor, e diante do seu exército: e levaram dali mui grande despojo.
14 Watu wa Yuda wakachukua nyara nyingi sana, wakaangamiza vijiji vyote vinavyoizunguka Gerari, kwa kuwa hofu ya Bwana ilikuwa imewaangukia. Wakateka nyara vijiji hivi vyote, kwani kulikuwepo nyara nyingi huko.
E feriram todas as cidades nos arredores de Gerar; porque o terror do Senhor estava sobre eles; e saquearam todas as cidades, porque havia nelas muita preza.
15 Pia wakashambulia kambi za wachunga makundi ya wanyama wakachukua na kuyaswaga makundi ya kondoo, mbuzi na ngamia. Kisha wakarudi Yerusalemu.
Também feriram as malhadas do gado; e levaram ovelhas em abundância, e camelos, e voltaram para Jerusalém.

< 2 Nyakati 14 >