< 2 Nyakati 14 >

1 Naye Abiya akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi.
Abija s'endormit avec ses pères, et on l'ensevelit dans la cité de David; et Asa son fils régna à sa place. De son temps, le pays fut en repos pendant dix ans.
2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Bwana Mungu wake.
Asa fit ce qui est bon et droit aux yeux de l'Éternel, son Dieu.
3 Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, akayavunja yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Maashera.
Il ôta les autels étrangers et les hauts lieux; il brisa les statues et mit en pièces les emblèmes d'Ashéra.
4 Akawaamuru Yuda kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao na kutii sheria zake na amri zake.
Et il recommanda à Juda de rechercher l'Éternel, le Dieu de leurs pères, et de pratiquer la loi et les commandements.
5 Akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu za kufukizia uvumba kwenye kila mji katika Yuda, nao ufalme ulikuwa na amani katika utawala wake.
Il ôta de toutes les villes de Juda les hauts lieux et les colonnes consacrées au soleil. Et le royaume fut en repos devant lui.
6 Akajenga miji yenye ngome katika Yuda, wakati nchi ikiwa na amani. Hakuna mtu yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa kuwa Bwana alimstarehesha.
Il bâtit des villes fortes en Juda; car le pays fut en repos; et pendant ces années-là il n'y eut point de guerre contre lui, parce que l'Éternel lui donna du repos.
7 Mfalme akawaambia Yuda, “Tuijenge hii miji na tuizungushie kuta, pamoja na minara, malango na makomeo. Nchi bado ni yetu, kwa sababu tumemtafuta Bwana Mungu wetu, tulimtafuta naye ametupa raha kila upande.” Hivyo wakajenga na wakafanikiwa.
Et il dit à Juda: Bâtissons ces villes, et environnons-les de murailles, de tours, de portes et de barres; le pays est encore devant nous, parce que nous avons recherché l'Éternel notre Dieu; nous l'avons recherché, et il nous a donné du repos de tous côtés. Ainsi ils bâtirent et prospérèrent.
8 Asa alikuwa na jeshi la watu 300,000 kutoka Yuda, wenye ngao kubwa na mikuki na jeshi la watu 280,000 kutoka Benyamini, wenye ngao ndogo na pinde. Watu hawa wote walikuwa wapiganaji mashujaa.
Or Asa avait une armée de trois cent mille hommes de Juda, portant le grand bouclier et la lance, et de deux cent quatre-vingt mille de Benjamin, portant le petit bouclier et tirant de l'arc, tous vaillants guerriers.
9 Zera Mkushi akatoka kupigana dhidi yao akiwa na jeshi la watu maelfu ya maelfu na magari ya vita 300, nao wakaja mpaka Maresha.
Mais Zérach, l'Éthiopien, sortit contre eux avec une armée d'un million d'hommes, et de trois cents chars; et il vint jusqu'à Marésha.
10 Asa akatoka kumkabili, nao wakapanga vita katika Bonde la Sefatha karibu na Maresha.
Et Asa alla au-devant de lui, et ils se rangèrent en bataille dans la vallée de Tséphatha, près de Marésha.
11 Kisha Asa akamlilia Bwana Mungu wake na kusema, “Ee Bwana, hakuna yeyote aliye kama wewe wa kuwasaidia wasio na nguvu dhidi ya wenye nguvu. Utusaidie, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, kwa kuwa tunakutumainia wewe, nasi kwa jina lako tumekuja dhidi ya jeshi hili kubwa. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, usiwaache wanadamu wakushinde wewe.”
Alors Asa cria à l'Éternel son Dieu, et dit: Éternel! Tu ne fais point de différence pour aider, que l'on soit nombreux ou sans force! Aide-nous, Éternel, notre Dieu! car nous nous sommes appuyés sur toi, et nous sommes venus en ton nom contre cette multitude. Tu es l'Éternel, notre Dieu: que l'homme ne prévale pas contre toi!
12 Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa na Yuda. Wakushi wakakimbia,
Et l'Éternel frappa les Éthiopiens devant Asa et devant Juda; et les Éthiopiens s'enfuirent.
13 naye Asa na jeshi lake wakawafuatia mpaka Gerari. Idadi kubwa ya Wakushi ilianguka hata wasiweze kuinuka tena, wakapondapondwa mbele za Bwana na majeshi yake.
Asa et le peuple qui était avec lui, les poursuivirent jusqu'à Guérar, et il tomba tant d'Éthiopiens, qu'ils ne purent se remettre; car ils furent écrasés devant l'Éternel et son armée, et on emporta un fort grand butin.
14 Watu wa Yuda wakachukua nyara nyingi sana, wakaangamiza vijiji vyote vinavyoizunguka Gerari, kwa kuwa hofu ya Bwana ilikuwa imewaangukia. Wakateka nyara vijiji hivi vyote, kwani kulikuwepo nyara nyingi huko.
Ils frappèrent toutes les villes autour de Guérar, car la terreur de l'Éternel était sur elles; et ils pillèrent toutes ces villes, car il s'y trouvait beaucoup de butin.
15 Pia wakashambulia kambi za wachunga makundi ya wanyama wakachukua na kuyaswaga makundi ya kondoo, mbuzi na ngamia. Kisha wakarudi Yerusalemu.
Ils frappèrent aussi les tentes des troupeaux, et emmenèrent des brebis et des chameaux en abondance; puis ils retournèrent à Jérusalem.

< 2 Nyakati 14 >