< 2 Nyakati 14 >

1 Naye Abiya akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi.
Abia se coucha avec ses pères, et on l'enterra dans la ville de David. Asa, son fils, régna à sa place; de son temps, le pays se reposa pendant dix ans.
2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Bwana Mungu wake.
Asa fit ce qui est bien et droit aux yeux de Yahweh, son Dieu. Il fit disparaître les autels de l'étranger et les hauts lieux,
3 Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, akayavunja yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Maashera.
il brisa les stèles et coupa les aschérahs.
4 Akawaamuru Yuda kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao na kutii sheria zake na amri zake.
Il ordonna à Juda de rechercher Yahweh, le Dieu de ses pères, et d'accomplir la loi et le précepte.
5 Akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu za kufukizia uvumba kwenye kila mji katika Yuda, nao ufalme ulikuwa na amani katika utawala wake.
Il fit disparaître de toutes les villes de Juda les hauts lieux et les statues; et le royaume fut en repos devant lui.
6 Akajenga miji yenye ngome katika Yuda, wakati nchi ikiwa na amani. Hakuna mtu yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa kuwa Bwana alimstarehesha.
Il bâtit des villes fortes en Juda; car le pays était en repos, et il n'y eut pas de guerre contre lui pendant ces années là, parce que Yahweh lui donna du repos.
7 Mfalme akawaambia Yuda, “Tuijenge hii miji na tuizungushie kuta, pamoja na minara, malango na makomeo. Nchi bado ni yetu, kwa sababu tumemtafuta Bwana Mungu wetu, tulimtafuta naye ametupa raha kila upande.” Hivyo wakajenga na wakafanikiwa.
Il dit à Juda: " Bâtissons ces villes, entourons-les de murs, de tours, de portes et de serrures; le pays est encore ouvert devant nous; car nous avons recherché Yahweh, notre Dieu; nous l'avons recherché, et il nous a donné du repos de tous cotés. " Ils bâtirent donc et réussirent.
8 Asa alikuwa na jeshi la watu 300,000 kutoka Yuda, wenye ngao kubwa na mikuki na jeshi la watu 280,000 kutoka Benyamini, wenye ngao ndogo na pinde. Watu hawa wote walikuwa wapiganaji mashujaa.
Asa avait une armée de trois cent mille hommes de Juda, portant le bouclier et la lance, et de deux cent quatre-vingt mille de Benjamin, portant le bouclier et tirant de l'arc, tous vaillants hommes.
9 Zera Mkushi akatoka kupigana dhidi yao akiwa na jeshi la watu maelfu ya maelfu na magari ya vita 300, nao wakaja mpaka Maresha.
Zara, l'éthiopien, sortit contre eux avec une armée d'un million d'hommes et trois cents chars, et il s'avança jusqu'à Marésa.
10 Asa akatoka kumkabili, nao wakapanga vita katika Bonde la Sefatha karibu na Maresha.
Asa sortit contre lui, et ils se rangèrent en bataille dans la vallée de Séphata, près de Marésa.
11 Kisha Asa akamlilia Bwana Mungu wake na kusema, “Ee Bwana, hakuna yeyote aliye kama wewe wa kuwasaidia wasio na nguvu dhidi ya wenye nguvu. Utusaidie, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, kwa kuwa tunakutumainia wewe, nasi kwa jina lako tumekuja dhidi ya jeshi hili kubwa. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, usiwaache wanadamu wakushinde wewe.”
Asa cria vers Yahweh, son Dieu, et dit: " Yahweh, vous pouvez secourir celui qui est faible aussi facilement que celui qui est fort; secourez-nous, Yahweh, notre Dieu! Car c'est sur vous que nous nous appuyons, et c'est en votre nom que nous sommes venus contre cette multitude. Yahweh, vous êtes notre Dieu: qu'un homme ne l'emporte pas contre vous! "
12 Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa na Yuda. Wakushi wakakimbia,
Yahweh frappa les Ethiopiens devant Asa et devant Juda, et les Ethiopiens prirent la fuite.
13 naye Asa na jeshi lake wakawafuatia mpaka Gerari. Idadi kubwa ya Wakushi ilianguka hata wasiweze kuinuka tena, wakapondapondwa mbele za Bwana na majeshi yake.
Asa et le peuple qui était avec lui les poursuivirent jusqu'à Gérare, et il tomba un si grand nombre d'Ethiopiens, qu'il n'y eut plus pour eux espoir de rétablissement, car ils furent brisés devant Yahweh et devant son camp. Asa et son peuple firent un très grand butin;
14 Watu wa Yuda wakachukua nyara nyingi sana, wakaangamiza vijiji vyote vinavyoizunguka Gerari, kwa kuwa hofu ya Bwana ilikuwa imewaangukia. Wakateka nyara vijiji hivi vyote, kwani kulikuwepo nyara nyingi huko.
ils frappèrent toutes les villes autour de Gérare, car la terreur de Yahweh était sur elles; ils pillèrent toutes les villes, car il s'y trouvait un grand butin.
15 Pia wakashambulia kambi za wachunga makundi ya wanyama wakachukua na kuyaswaga makundi ya kondoo, mbuzi na ngamia. Kisha wakarudi Yerusalemu.
Ils frappèrent aussi les tentes des troupeaux, et ils capturèrent un grand nombre de brebis et des chameaux; et ils s'en revinrent à Jérusalem.

< 2 Nyakati 14 >