< 2 Nyakati 14 >

1 Naye Abiya akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi.
Abija se coucha avec ses pères, et on l'enterra dans la ville de David; et Asa, son fils, régna à sa place. De son vivant, le pays fut tranquille pendant dix ans.
2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Bwana Mungu wake.
Asa fit ce qui est bon et droit aux yeux de l'Éternel, son Dieu.
3 Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, akayavunja yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Maashera.
Il fit disparaître les autels étrangers et les hauts lieux, brisa les colonnes, abattit les mâts d'ashère,
4 Akawaamuru Yuda kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao na kutii sheria zake na amri zake.
et ordonna à Juda de chercher l'Éternel, le Dieu de ses pères, et d'obéir à sa loi et à ses ordres.
5 Akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu za kufukizia uvumba kwenye kila mji katika Yuda, nao ufalme ulikuwa na amani katika utawala wake.
Il fit disparaître de toutes les villes de Juda les hauts lieux et les images du soleil, et le royaume fut tranquille devant lui.
6 Akajenga miji yenye ngome katika Yuda, wakati nchi ikiwa na amani. Hakuna mtu yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa kuwa Bwana alimstarehesha.
Il bâtit des villes fortes en Juda; car le pays était tranquille, et il n'y eut pas de guerre en ces années-là, parce que Yahvé lui avait donné du repos.
7 Mfalme akawaambia Yuda, “Tuijenge hii miji na tuizungushie kuta, pamoja na minara, malango na makomeo. Nchi bado ni yetu, kwa sababu tumemtafuta Bwana Mungu wetu, tulimtafuta naye ametupa raha kila upande.” Hivyo wakajenga na wakafanikiwa.
Car il dit à Juda: « Bâtissons ces villes et faisons des murs autour d'elles, avec des tours, des portes et des barres. Le pays est encore devant nous, car nous avons cherché Yahvé notre Dieu. Nous l'avons cherché, et il nous a donné du repos de tous côtés. » Ils construisirent donc et prospérèrent.
8 Asa alikuwa na jeshi la watu 300,000 kutoka Yuda, wenye ngao kubwa na mikuki na jeshi la watu 280,000 kutoka Benyamini, wenye ngao ndogo na pinde. Watu hawa wote walikuwa wapiganaji mashujaa.
Asa avait une armée de trois cent mille hommes de Juda, portant des boucliers et des lances, et de deux cent quatre-vingt mille hommes de Benjamin, portant des boucliers et tirant de l'arc. Tous ces hommes étaient de vaillants guerriers.
9 Zera Mkushi akatoka kupigana dhidi yao akiwa na jeshi la watu maelfu ya maelfu na magari ya vita 300, nao wakaja mpaka Maresha.
Zérah, l'Éthiopien, sortit contre eux avec une armée d'un million de soldats et trois cents chars, et il arriva à Maréscha.
10 Asa akatoka kumkabili, nao wakapanga vita katika Bonde la Sefatha karibu na Maresha.
Asa sortit à sa rencontre, et ils se rangèrent en bataille dans la vallée de Zephatha, à Maréscha.
11 Kisha Asa akamlilia Bwana Mungu wake na kusema, “Ee Bwana, hakuna yeyote aliye kama wewe wa kuwasaidia wasio na nguvu dhidi ya wenye nguvu. Utusaidie, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, kwa kuwa tunakutumainia wewe, nasi kwa jina lako tumekuja dhidi ya jeshi hili kubwa. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, usiwaache wanadamu wakushinde wewe.”
Asa cria à Yahvé, son Dieu, et dit: « Yahvé, il n'y a personne d'autre que toi pour nous aider, entre le puissant et le faible. Secours-nous, Yahvé notre Dieu, car nous comptons sur toi, et c'est en ton nom que nous sommes venus contre cette multitude. Yahvé, tu es notre Dieu. Ne laisse pas l'homme l'emporter sur toi ».
12 Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa na Yuda. Wakushi wakakimbia,
Et Yahvé frappa les Éthiopiens devant Asa et devant Juda, et les Éthiopiens s'enfuirent.
13 naye Asa na jeshi lake wakawafuatia mpaka Gerari. Idadi kubwa ya Wakushi ilianguka hata wasiweze kuinuka tena, wakapondapondwa mbele za Bwana na majeshi yake.
Asa et le peuple qui était avec lui les poursuivirent jusqu'à Gerar. Les Éthiopiens tombèrent en si grand nombre qu'ils ne purent se relever, car ils furent détruits devant Yahvé et devant son armée. L'armée de Juda emporta un très gros butin.
14 Watu wa Yuda wakachukua nyara nyingi sana, wakaangamiza vijiji vyote vinavyoizunguka Gerari, kwa kuwa hofu ya Bwana ilikuwa imewaangukia. Wakateka nyara vijiji hivi vyote, kwani kulikuwepo nyara nyingi huko.
Ils frappèrent toutes les villes des environs de Gerar, car la crainte de l'Éternel les saisit. Ils pillèrent toutes les villes, car il y avait là beaucoup de butin.
15 Pia wakashambulia kambi za wachunga makundi ya wanyama wakachukua na kuyaswaga makundi ya kondoo, mbuzi na ngamia. Kisha wakarudi Yerusalemu.
Ils frappèrent aussi les tentes de ceux qui avaient du bétail et emportèrent en abondance des moutons et des chameaux, puis ils retournèrent à Jérusalem.

< 2 Nyakati 14 >