< 2 Nyakati 14 >

1 Naye Abiya akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi.
Forsothe Abia slepte with hise fadris, and thei birieden hym in the citee of Dauid; and Asa, his sone, regnede for hym. In whos daies the lond restide ten yeer.
2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Bwana Mungu wake.
And Asa dide that, that was good and plesaunt in the siyt of his God, and he destriede the auteris of straunge worschipyng, and `he destriede hiy places,
3 Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, akayavunja yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Maashera.
and brak ymagis, and kittide doun woodis;
4 Akawaamuru Yuda kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao na kutii sheria zake na amri zake.
and he comaundide Juda to seke the Lord God of her fadris, and to do the lawe and alle comaundementis.
5 Akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu za kufukizia uvumba kwenye kila mji katika Yuda, nao ufalme ulikuwa na amani katika utawala wake.
And he took awei fro alle the citees of Juda auteris and templis of idols, and he regnede in pees.
6 Akajenga miji yenye ngome katika Yuda, wakati nchi ikiwa na amani. Hakuna mtu yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa kuwa Bwana alimstarehesha.
And he bildide stronge cytees in Juda; for he was in reste, and no batels risiden in his tymes, for the Lord yaf pees.
7 Mfalme akawaambia Yuda, “Tuijenge hii miji na tuizungushie kuta, pamoja na minara, malango na makomeo. Nchi bado ni yetu, kwa sababu tumemtafuta Bwana Mungu wetu, tulimtafuta naye ametupa raha kila upande.” Hivyo wakajenga na wakafanikiwa.
Forsothe he seide to Juda, Bilde we these cytees, and cumpasse we with wallis, and strengthe we with touris and yatis and lockis, as longe as alle thingis ben restful fro batel; for we han souyte the Lord God of oure fadris, and he hath youe to vs pees bi cumpas. Therfor thei bildiden, and no lettyng was in bildyng.
8 Asa alikuwa na jeshi la watu 300,000 kutoka Yuda, wenye ngao kubwa na mikuki na jeshi la watu 280,000 kutoka Benyamini, wenye ngao ndogo na pinde. Watu hawa wote walikuwa wapiganaji mashujaa.
Sotheli Asa hadde in his oost thre hundrid thousynde of men of Juda berynge scheldis and speris, sotheli of Beniamyn he hadde two hundrid thousynde and fourscoore thousynde of scheeld beeris and of archeris; alle these weren ful stronge men.
9 Zera Mkushi akatoka kupigana dhidi yao akiwa na jeshi la watu maelfu ya maelfu na magari ya vita 300, nao wakaja mpaka Maresha.
Forsothe Zara of Ethiop yede out ayens hem with his oost ten `sithis an hundrid thousynde, and with thre hundrid charis, and cam `til to Masera.
10 Asa akatoka kumkabili, nao wakapanga vita katika Bonde la Sefatha karibu na Maresha.
Certis Aza yede ayens hem, and araiede scheltrun to batel in the valei Sephata, which is bisidis Masera. And he inwardli clepide the Lord God,
11 Kisha Asa akamlilia Bwana Mungu wake na kusema, “Ee Bwana, hakuna yeyote aliye kama wewe wa kuwasaidia wasio na nguvu dhidi ya wenye nguvu. Utusaidie, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, kwa kuwa tunakutumainia wewe, nasi kwa jina lako tumekuja dhidi ya jeshi hili kubwa. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, usiwaache wanadamu wakushinde wewe.”
and seide, Lord, no dyuersitee is anentis thee, whether thou helpe in fewe, ethir in manye; oure Lord God, helpe thou vs, for we han trist in thee and in thi name, and camen ayens this multitude; Lord, thou art oure God, a man haue not the maistrye ayens thee.
12 Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa na Yuda. Wakushi wakakimbia,
Therfor the Lord made aferd Ethiopens bifor Asa and Juda, and Ethiopens fledden; and Asa and his puple,
13 naye Asa na jeshi lake wakawafuatia mpaka Gerari. Idadi kubwa ya Wakushi ilianguka hata wasiweze kuinuka tena, wakapondapondwa mbele za Bwana na majeshi yake.
that was with hym, pursuede hem `til to Gerare. And Ethiopens felden doun `til to deeth, for thei weren al to-brokun bi the Lord sleynge, and bi his oost fiytynge. Therfor thei token many spuylis,
14 Watu wa Yuda wakachukua nyara nyingi sana, wakaangamiza vijiji vyote vinavyoizunguka Gerari, kwa kuwa hofu ya Bwana ilikuwa imewaangukia. Wakateka nyara vijiji hivi vyote, kwani kulikuwepo nyara nyingi huko.
and smitiden alle the citees `bi the cumpas of Gerare; for greet drede hadde assailid alle men. And thei rifliden cytees, and baren a weye myche prey;
15 Pia wakashambulia kambi za wachunga makundi ya wanyama wakachukua na kuyaswaga makundi ya kondoo, mbuzi na ngamia. Kisha wakarudi Yerusalemu.
but also thei destrieden the fooldis of scheep, and token multitude without noumbre of scheep and of camels, and turneden ayen in to Jerusalem.

< 2 Nyakati 14 >