< 2 Nyakati 14 >

1 Naye Abiya akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi.
Then Abijah slept with his fathers, and they buried him in the City of David. And his son, Asa, reigned in his place. During his days, the land was quiet for ten years.
2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Bwana Mungu wake.
Now Asa did what was good and pleasing in the sight of his God. And he overturned the altars of foreign worship, and the high places.
3 Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, akayavunja yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Maashera.
And he broke apart the statues, and he cut down the sacred groves.
4 Akawaamuru Yuda kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao na kutii sheria zake na amri zake.
And he instructed Judah that they should seek the Lord, the God of their fathers, and that they should carry out the law and all the commandments.
5 Akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu za kufukizia uvumba kwenye kila mji katika Yuda, nao ufalme ulikuwa na amani katika utawala wake.
And he took away, from all the cities of Judah, the altars and the shrines. And he reigned in peace.
6 Akajenga miji yenye ngome katika Yuda, wakati nchi ikiwa na amani. Hakuna mtu yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa kuwa Bwana alimstarehesha.
Also, he built fortified cities in Judah. For it was quiet, and in his time no wars had arisen. For the Lord was generously granting peace.
7 Mfalme akawaambia Yuda, “Tuijenge hii miji na tuizungushie kuta, pamoja na minara, malango na makomeo. Nchi bado ni yetu, kwa sababu tumemtafuta Bwana Mungu wetu, tulimtafuta naye ametupa raha kila upande.” Hivyo wakajenga na wakafanikiwa.
Then he said to Judah: “Let us build these cities, and strengthen them with walls, and fortify them with towers and gates and bars, while all things are at rest from wars. For we have sought the Lord, the God of our fathers, and he has granted to us peace on every side.” And so they built, and there was nothing to impede them from building.
8 Asa alikuwa na jeshi la watu 300,000 kutoka Yuda, wenye ngao kubwa na mikuki na jeshi la watu 280,000 kutoka Benyamini, wenye ngao ndogo na pinde. Watu hawa wote walikuwa wapiganaji mashujaa.
Now Asa had in his army three hundred thousand men of Judah, carrying shields and spears, and truly, of Benjamin, two hundred eighty thousand men with shields and bows. All of these were very valiant men.
9 Zera Mkushi akatoka kupigana dhidi yao akiwa na jeshi la watu maelfu ya maelfu na magari ya vita 300, nao wakaja mpaka Maresha.
Then Zerah, the Ethiopian, went forth against them with his army of one million men, and three hundred chariots. And he approached as far as Mareshah.
10 Asa akatoka kumkabili, nao wakapanga vita katika Bonde la Sefatha karibu na Maresha.
And Asa traveled to meet him, and he set up a battle line for the war in the Valley of Zephathah, which is near Mareshah.
11 Kisha Asa akamlilia Bwana Mungu wake na kusema, “Ee Bwana, hakuna yeyote aliye kama wewe wa kuwasaidia wasio na nguvu dhidi ya wenye nguvu. Utusaidie, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, kwa kuwa tunakutumainia wewe, nasi kwa jina lako tumekuja dhidi ya jeshi hili kubwa. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, usiwaache wanadamu wakushinde wewe.”
And he called upon the Lord God, and he said: “O Lord, there is no difference to you, whether you assist by few, or by many. Help us, O Lord our God. For having faith in you and in your name, we have gone forth against this multitude. O Lord, you are our God. Do not allow man to prevail against you.”
12 Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa na Yuda. Wakushi wakakimbia,
And so the Lord terrified the Ethiopians before Asa and Judah. And the Ethiopians fled.
13 naye Asa na jeshi lake wakawafuatia mpaka Gerari. Idadi kubwa ya Wakushi ilianguka hata wasiweze kuinuka tena, wakapondapondwa mbele za Bwana na majeshi yake.
And Asa, and the people who were with him, pursued them as far as Gerar. And the Ethiopians fell, even unto utter destruction, for the Lord was striking, and his army was battling, and they were destroyed. Therefore, they took many spoils.
14 Watu wa Yuda wakachukua nyara nyingi sana, wakaangamiza vijiji vyote vinavyoizunguka Gerari, kwa kuwa hofu ya Bwana ilikuwa imewaangukia. Wakateka nyara vijiji hivi vyote, kwani kulikuwepo nyara nyingi huko.
And they struck all the cities surrounding Gerar. For indeed, a great fear had overwhelmed everyone. And they despoiled the cities, and they carried away much plunder.
15 Pia wakashambulia kambi za wachunga makundi ya wanyama wakachukua na kuyaswaga makundi ya kondoo, mbuzi na ngamia. Kisha wakarudi Yerusalemu.
Then too, destroying the fencing for the sheep, they took an innumerable multitude of cattle and camels. And they returned to Jerusalem.

< 2 Nyakati 14 >