< 2 Nyakati 13 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
W osiemnastym roku króla Jeroboama [zaczął] królować Abiasz nad Judą.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
Trzy lata królował w Jerozolimie, a jego matka [miała] na imię Maaka [i była] córką Uriela z Gibea. I trwała wojna między Abiaszem a Jeroboamem.
3 Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.
Abiasz więc przyszykował wojsko liczące czterysta tysięcy dzielnych wojowników, wyborowych mężczyzn. Jeroboam także przyszykował przeciwko niemu osiemset tysięcy wyborowych mężczyzn, dzielnych wojowników.
4 Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi!
Wtedy Abiasz stanął na szczycie góry Semaraim, [położonej] wśród gór Efraim, i powiedział: Słuchajcie mnie, Jeroboamie i cały Izraelu!
5 Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi?
Czy nie [powinniście] wiedzieć, że PAN, Bóg Izraela, dał Dawidowi panowanie nad Izraelem na wieki – jemu i jego synom – przymierzem soli?
6 Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake.
Lecz powstał Jeroboam, syn Nebata, sługa Salomona, syna Dawida, i zbuntował się przeciw swojemu panu.
7 Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.
I zebrali się u niego lekkomyślni mężczyźni, synowie Beliala, i wzmocnili się przeciw Roboamowi, synowi Salomona. A Roboam, będąc młodzieńcem i lękliwego serca, nie mógł się im mężnie oprzeć.
8 “Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu.
A wy teraz zamierzacie przeciwstawić się królestwu PANA, które jest w rękach synów Dawida; jesteście wielkim tłumem i [macie] ze sobą złote cielce, które Jeroboam wykonał wam jako bogów.
9 Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.
Czy nie odrzuciliście kapłanów PANA, synów Aarona, i Lewitów i czy nie ustanowiliście sobie kapłanów jak [inne] narody ziemi? Ktokolwiek przychodzi z młodym cielcem i siedmioma baranami, aby się poświęcić, staje się kapłanem tych, którzy nie [są] bogami.
10 “Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia.
Ale dla nas PAN jest naszym Bogiem i nie opuściliśmy go. Kapłani, którzy służą PANU, [są] synami Aarona, a Lewici pełnią swoje obowiązki.
11 Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu.
I każdego ranka i wieczora składają PANU w ofierze całopalenia i wonności oraz układają chleby pokładne na czystym stole, [przygotowują] także złoty świecznik i jego lampy, aby płonęły co wieczór. W ten oto sposób przestrzegamy rozkazu PANA, naszego Boga, ale wy go opuściliście.
12 Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”
Oto więc z nami na czele jest Bóg wraz ze swoimi kapłanami mającymi głośne trąby, aby grzmiały przeciwko wam. Synowie Izraela, nie walczcie z PANEM, Bogiem waszych ojców, bo wam się nie powiedzie.
13 Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma.
Tymczasem Jeroboam rozkazał uczynić zasadzkę i napaść ich od tyłu. I stali oni przed Judą, a zasadzka [była] na tyłach.
14 Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao,
Gdy [synowie] Judy zobaczyli, że walka [toczy się] z przodu i z tyłu, wołali do PANA, a kapłani zadęli w trąby.
15 nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda.
Mężczyźni Judy wydali też okrzyk. I kiedy wydali okrzyk, Bóg poraził Jeroboama i całego Izraela przed Abiaszem i Judą.
16 Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao.
I synowie Izraela uciekali przed Judą, ale Bóg wydał ich w ich ręce.
17 Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli.
I Abiasz i jego lud zadali im wielką klęskę, tak że spośród Izraela poległo pięćset tysięcy wyborowych mężczyzn.
18 Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
W tym czasie więc synowie Izraela zostali upokorzeni, a umocnili się synowie Judy, ponieważ polegali na PANU, Bogu swoich ojców.
19 Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo.
I Abiasz ścigał Jeroboama, i odebrał mu miasta: Betel, Jeszanę i Efron razem z należącymi do nich wioskami.
20 Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.
Jeroboam nie mógł powrócić już do sił za dni Abiasza i PAN poraził go tak, że umarł.
21 Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.
A Abiasz umocnił się i wziął sobie czternaście żon, i spłodził dwudziestu dwóch synów i szesnaście córek.
22 Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
Ale pozostałe dzieje Abiasza, jego czyny i słowa są zapisane w księdze proroka Iddo.

< 2 Nyakati 13 >