< 2 Nyakati 13 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
En la dix-huitième année du règne de Jéroboam, Abia régna sur Juda.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
Il régna trois ans à Jérusalem, et le nom de sa mère était Michaïa, fille d’Uriel de Gabaa; et il y eut guerre entre Abia et Jéroboam.
3 Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.
Et comme Abia préparait le combat, et qu’il avait des hommes très vaillants, et quatre cent mille guerriers choisis. Jéroboam rangea vis-à-vis en bataille une armée de huit cent mille hommes, qui eux aussi étaient très forts aux combats.
4 Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi!
Abia s’arrêta donc sur la montagne de Séméron, qui était en Ephraïm, et il dit: Ecoutez, Jéroboam, et tout Israël.
5 Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi?
Est-ce que vous ignorez que le Seigneur Dieu d’Israël a donné à David un royaume sur Israël pour toujours, à lui et à ses fils, par un pacte de sel?
6 Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake.
Et Jéroboam, fils de Nabath, serviteur de Salomon, fils de David, s’est levé et s’est révolté contre son seigneur;
7 Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.
Et se sont réunis à lui des hommes de néant, fils de Bélial, et ils ont prévalu contre Roboam, fils de Salomon: or Roboam était sans expérience, d’un cœur craintif, et il ne put leur résister.
8 “Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu.
Maintenant donc, vous dites que vous pourrez résister au royaume du Seigneur, qu’il possède par les fils de David, et que vous avez une grande multitude de peuple et des veaux d’or que Jéroboam vous a faits pour vos dieux.
9 Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.
Et vous avez chassé les prêtres du Seigneur, fils d’Aaron, et les Lévites; et vous vous êtes fait à vous-mêmes des prêtres comme tous les peuples de la terre: quiconque vient, et consacre sa main avec un taureau d’entre les bœufs, et avec sept béliers, est fait prêtre de ceux qui ne sont point dieux.
10 “Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia.
Mais notre Seigneur est Dieu, et nous ne l’abandonnons pas: des prêtres d’entre les fils d’Aaron servent le Seigneur, et les Lévites sont à leur place.
11 Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu.
On offre aussi des holocaustes au Seigneur chaque jour, le soir et le matin, ainsi qu’un parfum composé selon les préceptes de la loi, et l’on expose des pains sur la table très pure; nous avons le chandelier d’or et ses lampes, pour qu’elles soient toujours allumées le soir: car nous, nous gardons fidèlement les préceptes du Seigneur notre Dieu, que vous, vous avez abandonné.
12 Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”
Ainsi dans notre armée, le chef, c’est Dieu, et ses prêtres qui sonnent des trompettes, et les font retentir contre vous. Enfants d’Israël, ne combattez point contre le Seigneur Dieu de vos pères; car cela ne vous est point avantageux.
13 Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma.
Pendant qu’il disait ces choses. Jéroboam lui tendait par derrière des embûches; et, comme il se tenait en face des ennemis, il entourait de son armée Juda qui l’ignorait.
14 Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao,
Mais Juda, ayant tourné la tête, vit que la guerre le menaçait par devant et par derrière; et il cria vers le Seigneur, et les prêtres commencèrent à sonner des trompettes.
15 nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda.
Alors tous les hommes de Juda poussèrent de grands cris; or voici que, comme ils criaient, Dieu épouvanta Jéroboam et tout Israël, qui se trouvait en face d’Abia et de Juda.
16 Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao.
Ainsi les enfants d’Israël s’enfuirent devant Juda, et Dieu les livra en sa main.
17 Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli.
Abia les frappa, donc ainsi que son peuple, d’une grande plaie, et il tomba, blessés, du côté d’Israël, cinq cent mille des hommes forts.
18 Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
Et les enfants d’Israël furent humiliés en ce temps-là, et les enfants de Juda reprirent entièrement courage, parce qu’ils avaient espéré dans le Seigneur Dieu de leurs pères.
19 Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo.
Or Abia poursuivit Jéroboam fuyant, et il prit de ses villes: Béthel et ses filles, Jésana avec ses filles, Ephron aussi et ses filles.
20 Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.
Et Jéroboam ne fut plus assez fort pour résister dans les jours d’Abia; Dieu le frappa, et il mourut.
21 Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.
Ainsi Abia, son empire affermi, prit quatorze femmes, et procréa vingt-deux fils et seize filles.
22 Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
Le reste des actions, des voies et des œuvres d’Abia est écrit très exactement dans le livre d’Addo, le prophète.

< 2 Nyakati 13 >