< 2 Nyakati 13 >
1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
La dix-huitième année du roi Jéroboam, Abija commença à régner sur Juda.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
Il régna trois ans à Jérusalem. Sa mère s'appelait Micaja, fille d'Uriel, de Guibea. Or il y eut guerre entre Abija et Jéroboam.
3 Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.
Abija engagea la guerre avec une armée de vaillants guerriers, quatre cent mille hommes d'élite; et Jéroboam se rangea en bataille contre lui avec huit cent mille hommes d'élite, vaillants guerriers.
4 Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi!
Et Abija se tint sur la montagne de Tsémaraïm, qui est dans la montagne d'Éphraïm, et dit: Jéroboam et tout Israël, écoutez-moi!
5 Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi?
Ne devez-vous pas savoir que l'Éternel, le Dieu d'Israël, a donné pour toujours la royauté sur Israël, à David, à lui et à ses fils, par une alliance inviolable!
6 Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake.
Mais Jéroboam, fils de Nébat, serviteur de Salomon, fils de David, s'est élevé, et s'est révolté contre son seigneur;
7 Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.
Et des gens de rien, des misérables se sont joints à lui et se sont fortifiés contre Roboam, fils de Salomon. Or Roboam était un enfant et de faible courage, et il ne tint pas devant eux.
8 “Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu.
Et maintenant, vous pensez tenir devant la royauté de l'Éternel, qui est entre les mains des fils de David; et vous êtes une grande multitude, et vous avez avec vous les veaux d'or que Jéroboam vous a faits pour être vos dieux.
9 Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.
N'avez-vous pas repoussé les sacrificateurs de l'Éternel, les fils d'Aaron, et les Lévites? Et ne vous êtes-vous pas fait des sacrificateurs à la façon des peuples des autres pays? Quiconque est venu, pour être consacré, avec un jeune taureau et sept béliers, est devenu sacrificateur de ce qui n'est pas Dieu.
10 “Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia.
Mais pour nous, l'Éternel est notre Dieu, et nous ne l'avons point abandonné; les sacrificateurs qui font le service de l'Éternel, sont enfants d'Aaron, et ce sont les Lévites qui fonctionnent,
11 Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu.
Faisant fumer pour l'Éternel, chaque matin et chaque soir, les holocaustes et le parfum d'aromates. Les pains de proposition sont rangés sur la table pure, et on allume le chandelier d'or, avec ses lampes, chaque soir. Car nous gardons ce que l'Éternel notre Dieu veut qu'on garde; mais vous, vous l'avez abandonné.
12 Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”
Voici, Dieu et ses sacrificateurs sont avec nous, à notre tête, et les trompettes au son éclatant, pour les faire retentir contre vous. Enfants d'Israël, ne combattez pas contre l'Éternel, le Dieu de vos pères; car cela ne vous réussira point.
13 Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma.
Mais Jéroboam fit faire un détour à une embuscade, pour arriver derrière eux. Ainsi les Israélites étaient en face de Juda, et l'embuscade était derrière ceux-ci.
14 Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao,
Ceux de Juda regardèrent donc, et voici, ils avaient la bataille en face et par-derrière. Alors ils crièrent à l'Éternel, et les sacrificateurs sonnèrent des trompettes.
15 nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda.
Et tous les hommes de Juda poussèrent un cri de guerre, et au cri de guerre des hommes de Juda, Dieu frappa Jéroboam et tout Israël devant Abija et Juda;
16 Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao.
Et les enfants d'Israël s'enfuirent devant ceux de Juda, et Dieu les livra entre leurs mains.
17 Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli.
Abija et son peuple en firent un grand carnage, et il tomba d'Israël cinq cent mille hommes d'élite blessés à mort.
18 Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
Ainsi les enfants d'Israël furent humiliés en ce temps-là; et les enfants de Juda devinrent forts, parce qu'ils s'étaient appuyés sur l'Éternel, le Dieu de leurs pères.
19 Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo.
Or Abija poursuivit Jéroboam, et lui prit ces villes: Béthel et les villes de son ressort, Jeshana et les villes de son ressort, Éphron et les villes de son ressort.
20 Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.
Jéroboam n'eut plus de force pendant le temps d'Abija; et l'Éternel le frappa, et il mourut.
21 Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.
Mais Abija devint puissant. Il prit quatorze femmes, et engendra vingt-deux fils et seize filles.
22 Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
Le reste des actions d'Abija, et sa conduite, et ses paroles sont écrites dans les mémoires du prophète Iddo.