< 2 Nyakati 13 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
La dix-huitième année du roi Jéroboam, Abija commença à régner sur Juda.
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
Il régna trois ans à Jérusalem. Sa mère s'appelait Micaia, fille d'Uriel, de Guibea. Il y eut une guerre entre Abija et Jéroboam.
3 Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.
Abija se mit en campagne avec une armée de vaillants guerriers, quatre cent mille hommes d'élite, et Jéroboam se rangea en bataille contre lui avec huit cent mille hommes d'élite, qui étaient de vaillants guerriers.
4 Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi!
Abija se tint debout sur la montagne de Zemaraïm, qui est dans la montagne d'Ephraïm, et dit: « Écoute-moi, Jéroboam et tout Israël!
5 Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi?
Ne savez-vous pas que Yahvé, le Dieu d'Israël, a donné le royaume d'Israël à David pour toujours, à lui et à ses fils, par une alliance de sel?
6 Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake.
Mais Jéroboam, fils de Nebat, serviteur de Salomon, fils de David, se leva et se révolta contre son maître.
7 Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.
Des hommes sans valeur se rassemblèrent auprès de lui, des méchants qui se fortifièrent contre Roboam, fils de Salomon, alors que Roboam était jeune et avait le cœur tendre, et qu'il ne put leur résister.
8 “Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu.
« Maintenant, vous avez l'intention de résister au royaume de Yahvé entre les mains des fils de David. Vous êtes une grande multitude, et les veaux d'or que Jéroboam vous a faits pour dieux sont avec vous.
9 Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.
N'avez-vous pas chassé les prêtres de Yahvé, les fils d'Aaron et les Lévites, et ne vous êtes-vous pas fait des prêtres selon les coutumes des peuples d'autres pays? Celui qui vient se consacrer avec un jeune taureau et sept béliers peut être prêtre de ceux qui ne sont pas des dieux.
10 “Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia.
« Quant à nous, Yahvé est notre Dieu, et nous ne l'avons pas abandonné. Nous avons des prêtres au service de Yahvé, les fils d'Aaron, et les Lévites à leur service.
11 Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu.
Ils brûlent à Yahvé, chaque matin et chaque soir, des holocaustes et des parfums doux. Ils mettent aussi les pains de proposition en ordre sur la table pure, et prennent soin du chandelier d'or avec ses lampes, pour qu'elles brûlent chaque soir; car nous observons les instructions de l'Éternel, notre Dieu, mais vous l'avez abandonné.
12 Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”
Voici, Dieu est avec nous à notre tête, et ses prêtres avec les trompettes d'alarme pour sonner l'alarme contre vous. Enfants d'Israël, ne luttez pas contre Yahvé, le Dieu de vos pères, car vous ne réussirez pas. »
13 Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma.
Mais Jéroboam fit dresser une embuscade derrière eux; ils étaient donc devant Juda, et l'embuscade était derrière eux.
14 Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao,
Lorsque Juda regarda en arrière, voici, la bataille était devant et derrière eux; ils crièrent à Yahvé, et les prêtres sonnèrent des trompettes.
15 nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda.
Alors les hommes de Juda poussèrent des cris de guerre. Comme les hommes de Juda criaient, Dieu frappa Jéroboam et tout Israël devant Abija et Juda.
16 Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao.
Les enfants d'Israël s'enfuirent devant Juda, et Dieu les livra entre leurs mains.
17 Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli.
Abija et son peuple leur firent subir une grande défaite, et cinq cent mille élus d'Israël tombèrent morts.
18 Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
C'est ainsi que les enfants d'Israël furent soumis en ce temps-là et que les enfants de Juda l'emportèrent, car ils s'en remettaient à Yahvé, le Dieu de leurs pères.
19 Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo.
Abija poursuivit Jéroboam et lui prit des villes: Béthel et ses villages, Jeshanah et ses villages, et Ephron et ses villages.
20 Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.
Jéroboam ne recouvra pas ses forces du temps d'Abija. Yahvé le frappa, et il mourut.
21 Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.
Mais Abija devint puissant et prit pour lui quatorze femmes, et il engendra vingt-deux fils et seize filles.
22 Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
Le reste des actes d'Abija, sa conduite et ses paroles sont écrits dans le commentaire du prophète Iddo.

< 2 Nyakati 13 >