< 2 Nyakati 13 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
Yn the eiytenthe yeer of kyng Jeroboam Abia regnede on Juda;
2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
he regnede thre yeer in Jerusalem; and the name of hise modir was Mychaie, the douyter of Vriel of Gabaa. And batel was bitwixe Abia and Jeroboam.
3 Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.
And whanne Abia hadde bigunne batel, and hadde most chyualrouse men, and four hundrid thousynde of chosun men, Jeroboam arayede ayenward the scheltroun with eiyte hundrid thousynde of men, and thei weren chosun men and most stronge to batels.
4 Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi!
Therfor Abia stood on the hil Semeron, that was in Effraym, and seide, Here thou, Jeroboam and al Israel;
5 Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi?
whether ye knowen not, that the Lord God of Israel yaf to Dauid the rewme on Israel with outen ende, to hym and to hise sones in to the couenaunt of salt, `that is, stidefast and stable?
6 Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake.
And Jeroboam, the sone of Nabath, the seruaunt of Salomon, sone of Dauid, roos, and rebellide ayens his lord.
7 Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.
And most veyn men and the sones of Belial weren gaderid to hym, and thei hadden myyt ayens Roboam, the sone of Salomon. Certis Roboam was buystuouse, `ether fonne, and of feerdful herte, and myyte not ayenstonde hem.
8 “Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu.
Now therfor ye seien, that ye moun ayenstonde the rewme of the Lord, which he holdith in possessioun bi the sones of Dauid; and ye han a greet multitude of puple, and goldun caluys, whiche Jeroboam made in to goddis to you.
9 Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.
And ye han caste a wei the preestis of the Lord, the sones of Aaron, and dekenes, and ye han maad preestis to you, as alle the puplis of londis han preestis; who euer cometh and halewith his hond in a bole, in oxis, and in seuene wetheris, anoon he is maad preest of hem that ben not goddis.
10 “Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia.
But oure Lord is God, whom we forsaken not; and preestis of the sones of Aaron mynystren to the Lord, and dekenes ben in her ordre;
11 Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu.
and thei offren brent sacrifices to the Lord bi ech dai in the morewtid and euentid, and encense maad bi comaundementis of the lawe; and loues ben set forth in a moost clene boord; and at vs is the goldun candilstik and his lanterne, that it be teendid euere at euentid; forsothe we kepen the comaundementis of our God, whom ye han forsake.
12 Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”
Therfor God is duyk in oure oost, and hise preestis, that trumpen and sownen ayens you; nyle ye, sones of Israel, fiyte ayens the Lord God of youre fadris, for it spedith not to you.
13 Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma.
While he spak these thingis, Jeroboam made redi tresouns bihynde; and whanne he stood euene ayens the enemyes, he cumpasside with his oost Juda vnwitynge.
14 Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao,
And Juda bihelde, and siy batel neiy euene ayens, and bihynde the bak; and he criede to the Lord, and preestis bigunnen for to trumpe.
15 nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda.
And alle the men of Juda crieden, and, lo! while thei crieden, God made aferd Jeroboam and al Israel, that stood euen ayens Juda and Abia.
16 Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao.
And the men of Israel fledden fro Juda, and God bitook hem in to the hondis of men of Juda.
17 Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli.
Therfor Abia and his puple smoot hem with a greet wounde, and there felden doun of hem fyue hundrid thousynde of stronge men woundid.
18 Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
And the sones of Israel weren maad lowe in that tyme, and the sones of Juda weren coumfortid ful greetli, for thei hadden hopid in the Lord God of her fadris.
19 Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo.
Forsothe Abia pursuede Jeroboam fleynge, and took hise cytees, Bethel and hise vilagis, and Jesana with hise vilagis, and Ephron and hise vilagis;
20 Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.
and Jeroboam miyte no more ayenstonde in the daies of Abia, whom the Lord smoot, and he was deed.
21 Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.
Therfor Abia, whanne his empire was coumforted, took fourtene wyues, and he gendride two and twenti sones, and sixtene douytris.
22 Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.
The residue of wordis of Abia and of his weyes and werkis, ben writun ful diligentli in the book of Abdo, the profete.

< 2 Nyakati 13 >