< 2 Nyakati 12 >

1 Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mungu.
Et lorsque le royaume de Roboam fut fortifié et affermi, il abandonna la loi du Seigneur, lui et tout Israël avec lui.
2 Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu.
Mais à la cinquième année du règne de Roboam, Sésac, roi d’Égypte, monta à Jérusalem (parce que les Israélites avaient péché contre le Seigneur)
3 Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri.
Avec mille et deux cents chariots et soixante mille cavaliers; et le bas peuple qui était venu d’Égypte avec lui était sans nombre; il se composait de Libyens, de Troglodytes et d’Ethiopiens.
4 Akateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.
Et il prit les villes les plus fortifiées dans Juda, et il vint jusqu’à Jérusalem.
5 Ndipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’”
Or Séméias, le prophète, vint trouver le roi Roboam et les princes de Juda, qui s’étaient réunis à Jérusalem, fuyant Sésac, et il leur dit: Voici ce que dit le Seigneur: Vous, vous m’avez abandonné, et moi, je vous ai abandonnés à la main de Sésac.
6 Viongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mungu ni mwenye haki.”
Alors, consternés, les princes d’Israël et le roi dirent: Il est juste, le Seigneur.
7 Bwana Mungu alipoona kwamba wamejinyenyekeza, neno hili la Bwana likamjia Shemaya: “Maadamu wamejinyenyekeza, sitawaangamiza bali hivi karibuni nitawapatia wokovu. Ghadhabu yangu haitamwagwa juu ya Yerusalemu kwa kupitia Shishaki.
Et lorsque le Seigneur vit qu’ils étaient humiliés, la parole du Seigneur fut adressée à Séméias, disant: Puisqu’ils se sont humiliés, je ne les exterminerai point, je leur donnerai un peu de secours, et ma fureur ne s’épanchera pas sur Jérusalem par la main de Sésac;
8 Hata hivyo, watamtumikia Shishaki ili wapate kujifunza tofauti kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa nchi nyingine.”
Cependant ils le serviront, afin qu’ils sachent la différence de mon service et du service du royaume des nations.
9 Shishaki mfalme wa Misri alipoishambulia Yerusalemu, alichukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
C’est pourquoi Sésac, roi d’Égypte, se retira de Jérusalem après avoir enlevé les trésors de la maison du Seigneur et de la maison du roi, et il emporta tout avec lui, même les boucliers d’or qu’avait faits Salomon,
10 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
À la place desquels le roi en fit d’airain, et les remit aux chefs des scutaires qui gardaient le vestibule du palais.
11 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana walinzi walikwenda pamoja naye wakiwa wamebeba hizo ngao na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
Et lorsque le roi entrait dans la maison du Seigneur, les scutaires venaient et les prenaient, puis ils les reportaient de nouveau dans leur arsenal.
12 Kwa sababu Rehoboamu alijinyenyekeza, hasira ya Bwana ikageukia mbali naye, hakuangamizwa kabisa. Kukawa na hali nzuri katika Yuda.
Ainsi donc, parce qu’ils s’étaient humiliés, la colère du Seigneur fut détournée d’eux, et ils ne furent pas entièrement détruits, attendu qu’il se trouva encore dans Juda de bonnes œuvres.
13 Mfalme Rehoboamu akajiweka imara katika Yerusalemu na akaendelea kuwa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na saba, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili aliweke Jina lake humo. Mama yake aliitwa Naama, alikuwa Mwamoni.
Le roi Roboam se fortifia donc dans Jérusalem, et y régna; or il avait quarante et un ans quand il commença à régner, et il régna dix-sept ans à Jérusalem, ville que le Seigneur avait choisie d’entre toutes les tribus d’Israël pour y établir son nom: or le nom de sa mère était Naama, l’Ammanite.
14 Rehoboamu akatenda maovu kwa sababu hakuuelekeza moyo wake katika kumtafuta Bwana Mungu.
Mais il fit le mal, et ne prépara point son cœur pour chercher le Seigneur.
15 Kwa habari ya matukio katika utawala wa Rehoboamu, tangu mwanzo mpaka mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Shemaya na mwonaji Ido zinazohusiana na vizazi? Kulikuwako na vita mara kwa mara kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
Or les actions de Roboam, les premières et les dernières, sont écrites dans les livres de Séméias, le prophète, et d’Addo, le Voyant, et rapportées exactement: et Roboam et Jéroboam se firent la guerre durant tous leurs jours.
16 Rehoboamu akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et Roboam dormit avec ses pères, et il fut enseveli dans la cité de David; et Abia, son fils, régna en sa place.

< 2 Nyakati 12 >