< 2 Nyakati 10 >

1 Rehoboamu akaenda Shekemu, kwa kuwa Waisraeli wote walikuwa wamekwenda huko kumfanya yeye kuwa mfalme.
Et Roboam s'en alla à Sichem, parce que tout Israël était venu à Sichem pour l'établir Roi.
2 Yeroboamu mwana wa Nebati aliposikia hili (alikuwa bado yuko Misri alikokuwa amekimbilia awe mbali na Mfalme Solomoni), akarudi kutoka Misri.
Or il arriva que quand Jéroboam fils de Nébat, qui était en Egypte, où il s'en était fui de devant le Roi Salomon, l'eut appris, il revint d'Egypte.
3 Kwa hiyo wakatuma watu kumwita Yeroboamu, yeye na kusanyiko lote la Israeli wakamwendea Rehoboamu na kumwambia,
Car on l'avait envoyé appeler. Ainsi Jéroboam et tout Israël vinrent et parlèrent à Roboam, en disant:
4 “Baba yako aliweka nira nzito, lakini sasa tupunguzie kazi za kikatili na nira nzito aliyoweka juu yetu, nasi tutakutumikia.”
Ton père a mis sur nous un pesant joug, mais toi allège maintenant cette rude servitude de ton père, et ce pesant joug, qu'il a mis sur nous, et nous te servirons.
5 Rehoboamu akajibu, “Nendeni kwa muda wa siku tatu na kisha mnirudie.” Basi watu wakaenda zao.
Et il leur répondit: Retournez auprès de moi dans trois jours; et le peuple s'en alla.
6 Kisha Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee ambao walimtumikia Solomoni baba yake wakati wa uhai wake akawauliza, “Mnanishauri nini katika kuwajibu watu hawa?”
Et le Roi Roboam demanda conseil aux vieillards qui avaient été auprès de Salomon son père lorsqu'il vivait, et leur dit: Comment, et quelle chose me conseillez-vous de répondre à ce peuple?
7 Wakajibu, “Kama leo utakuwa mtumishi wa watu hawa na kuwahudumia na kuwapa jibu linaloridhisha, watakuwa watumishi wako daima.”
Et ils lui dirent: Si tu agis avec bonté envers ce peuple, que tu leur complaises, et que tu leur parles doucement, ils te seront serviteurs à toujours.
8 Lakini Rehoboamu akakataa shauri alilopewa na wazee na akataka ushauri kwa vijana wanaume rika lake waliokuwa wakimtumikia.
Mais il laissa le conseil que les vieillards lui avaient donné, et demanda conseil aux jeunes gens qui avaient été nourris avec lui, [et] qui étaient auprès de lui.
9 Akawauliza, “Ninyi ushauri wenu ni nini? Tutawajibuje watu hawa wanaoniambia, ‘Ifanye nyepesi nira baba yako aliyoweka juu yetu?’”
Et il leur dit: Que me conseillez-vous de répondre à ce peuple qui m'a dit: Allège le joug que ton père a mis sur nous?
10 Wale vijana wa rika lake wakamjibu, “Waambie watu hawa waliokuambia, ‘Baba yako aliweka nira nzito juu yetu, lakini ifanye nira yetu nyepesi,’ kuwa, ‘Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.
Et les jeunes gens qui avaient été nourris avec lui, lui répondirent, en disant: Tu diras ainsi à ce peuple qui t'a parlé, et t'a dit: Ton père a mis sur nous un pesant joug, mais toi allège-le-nous; tu leur répondras donc ainsi: Ce qu'il y a de plus petit en moi, est plus gros que les reins de mon père.
11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, mimi nitaifanya hata iwe nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi; mimi nitawachapa kwa nge.’”
Or mon père a mis sur vous un pesant joug, mais moi je rendrai votre joug encore plus pesant; mon père vous a châtiés avec des verges, mais moi [je vous châtierai] avec des fouets.
12 Siku tatu baadaye, Yeroboamu na watu wote wakamrudia Rehoboamu, kama mfalme alivyokuwa amesema, “Rudini kwangu baada ya siku tatu.”
Trois jours après Jéroboam, avec tout le peuple vint vers Roboam, selon que le Roi leur avait dit: Retournez vers moi dans trois jours.
13 Mfalme akawajibu watu kwa ukatili. Akikataa shauri alilopewa na wazee,
Mais le Roi leur répondit rudement; car le Roi Roboam négligea le conseil des vieillards.
14 akafuata shauri la vijana wa rika lake na kusema, “Baba yangu alifanya nira yenu kuwa nzito, mimi nitaifanya kuwa nzito zaidi. Baba yangu aliwachapa kwa mijeledi, mimi nitawachapa kwa nge.”
Et il leur parla selon le conseil des jeunes gens, en disant: Mon père a mis sur vous un pesant joug, mais moi je rendrai votre joug encore plus pesant; mon père vous a châtiés avec des verges, mais moi [je vous châtierai] avec des fouets.
15 Kwa hiyo mfalme hakuwasikiliza watu, kwa kuwa jambo hili lilitoka kwa Mungu ili kutimiza neno ambalo Bwana alikuwa amenena kwa Yeroboamu mwana wa Nebati kupitia Ahiya Mshiloni.
Le Roi donc n'écouta point le peuple, car cela était conduit par Dieu, afin que l'Eternel ratifiât sa parole, qu'il avait prononcée à Jéroboam fils de Nébat, par le moyen d'Ahija Silonite.
16 Israeli wote walipoona kuwa mfalme amekataa kuwasikiliza, wakamjibu mfalme: “Tuna fungu gani kwa Daudi? Sisi hatuna urithi kwa mwana wa Yese. Nendeni kwenye mahema yenu, ee Israeli, angalia nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wakaenda kwenye mahema yao.
Et quand tout Israël eut vu que le Roi ne les avait point écoutés, le peuple répondit au Roi, en disant: Quelle part avons-nous en David? Nous n'avons point d'héritage au fils d'Isaï; Israël, que chacun se retire en ses tentes; et toi David, pourvois maintenant à ta maison. Ainsi tout Israël s'en alla en ses tentes.
17 Lakini kwa habari ya Waisraeli waliokuwa wakiishi katika miji ya Yuda, Rehoboamu akaendelea kuwatawala bado.
Mais quant aux enfants d'Israël qui demeuraient dans les villes de Juda, Roboam régna sur eux.
18 Mfalme Rehoboamu akamtuma Adoniramu aliyekuwa msimamizi wa wale waliofanya kazi ngumu kwa kulazimishwa, lakini Israeli wote wakampiga kwa mawe hadi akafa. Hata hivyo, Mfalme Rehoboamu, akafanikiwa kuingia kwenye gari lake na kutorokea Yerusalemu.
Alors le Roi Roboam envoya Hadoram, qui était commis sur les tributs; mais les enfants d'Israël l'assommèrent de pierres, et il mourut. Et le Roi Roboam se hâta de monter sur un chariot, et s'enfuit à Jérusalem.
19 Hivyo Israeli wakaasi dhidi ya nyumba ya Daudi hadi leo.
Ainsi Israël se rebella contre la maison de David, jusqu'à aujourd'hui.

< 2 Nyakati 10 >