< 2 Nyakati 1 >
1 Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwa Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno.
Solomon son of David was strengthened in his rule, and Yahweh his God was with him and made him very powerful.
2 Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa.
Solomon spoke to all Israel, to the commanders of thousands and of hundreds, and to the judges, and to every prince in all Israel, the heads of the fathers' houses.
3 Naye Solomoni na kusanyiko lote wakakwea mpaka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kwa kuwa huko ndiko Hema la Kukutania la Mungu lilipokuwa, ambalo Mose mtumishi wa Bwana alikuwa amelitengeneza huko jangwani.
So Solomon and all the assembly with him went to the high place that was at Gibeon, for there was the tent of meeting of God, which Moses the servant of Yahweh, had made in the wilderness.
4 Basi Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu mpaka mahali alipokuwa amepatengeneza kwa ajili yake, kwa sababu alikuwa amesimamisha hema kwa ajili ya hilo Sanduku huko Yerusalemu.
But David had brought up the ark of God from Kiriath Jearim to the place that he had prepared for it, for he had pitched a tent for it in Jerusalem.
5 Lakini yale madhabahu ya shaba ambayo Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, alikuwa ametengeneza yalikuwa huko Gibeoni mbele ya Maskani ya Bwana Mungu, hivyo Solomoni na kusanyiko lote walimtafuta Mungu huko.
In addition, the bronze altar made by Bezalel son of Uri son of Hur was there before the tabernacle of Yahweh; Solomon and the assembly went to it.
6 Solomoni akapanda huko yalikokuwa madhabahu ya shaba mbele za Bwana katika Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu 1,000 za sadaka za kuteketezwa juu yake.
Solomon went up there to the bronze altar before Yahweh, which was at the tent of meeting, and offered one thousand burnt offerings on it.
7 Usiku ule Mungu akamtokea Solomoni na kumwambia, “Omba lolote utakalo nikupe.”
God appeared to Solomon that night and said to him, “Ask! What should I give you?”
8 Solomoni akamjibu Mungu, “Umemwonyesha baba yangu Daudi fadhili nyingi, nawe umeniweka niwe mfalme mahali pake.
Solomon said to God, “You have shown great covenant faithfulness to David my father, and have made me king in his place.
9 Sasa, Bwana Mungu, ahadi yako kwa baba yangu Daudi na ithibitike, kwa kuwa umenifanya mimi mfalme juu ya watu ambao ni wengi kama mavumbi ya nchi.
Now, Yahweh God, let your promise to David my father be carried out, for you have made me king over a people as numerous as the dust of the earth.
10 Nakuomba unipe mimi hekima na maarifa, ili niweze kuongoza watu hawa, kwa kuwa ni nani awezaye kutawala hawa watu wako walio wengi hivi?”
Now give me wisdom and knowledge, so that I may lead this people, for who can judge your people, who are so many in number?”
11 Mungu akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa jambo hili ndilo shauku ya moyo wako na hukuomba mali, utajiri au heshima, wala kifo kwa ajili ya adui zako, nawe kwa kuwa hukuomba maisha marefu, bali umeomba hekima na maarifa ili kuongoza watu wangu ambao nimekufanya uwe mfalme juu yao,
God said to Solomon, “Because this was in your heart, and because you have not asked for riches, wealth, or honor, nor for the life of those who hate you, nor for long life for yourself, but you have asked for wisdom and knowledge for yourself, so that you might rule my people, over whom I have made you king, and this is what I will do.
12 kwa hiyo utapewa hekima na maarifa. Tena nitakupa pia mali, utajiri na heshima, ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekuwepo kabla yako amewahi kuwa navyo, na hakuna yeyote baada yako atakayekuwa navyo.”
I will now give you wisdom and knowledge. I will also give you riches, wealth, and honor, as none of the kings had before you, and none after you will have.”
13 Ndipo Solomoni akaenda mpaka Yerusalemu kutoka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kutoka mbele ya Hema la Kukutania. Naye akatawala Israeli.
So Solomon came to Jerusalem from the high place that was at Gibeon, from before the tent of meeting; he reigned over Israel.
14 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
Solomon gathered chariots and horsemen, and he had 1,400 chariots and twelve thousand horsemen that he placed in the chariot cities, and with himself, the king in Jerusalem.
15 Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
The king made silver and gold as common in Jerusalem as the stones, and he made cedar wood as common as the sycamore trees that are in the lowlands.
16 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
As for the importation of horses from Egypt and Kue for Solomon, his merchants bought them from Kue at a price.
17 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha, na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
They imported a chariot from Egypt for six hundred shekels of silver, and a horse for 150 shekels. They also exported them to the kings of the Hittites and the Arameans.