< 1 Timotheo 1 >

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.
Paul, an apostle of Jesus Christ, according to a command of God our Savior, and of the Lord Jesus Christ our hope,
2 Kwa Timotheo, mwanangu halisi katika imani: Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timotheus—genuine child in faith: Grace, kindness, peace, from God our Father and Christ Jesus our Lord!
3 Kama nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia, endelea kubaki Efeso, ili kwamba upate kuwaagiza watu wasiendelee kufundisha mafundisho ya uongo
According as I exhorted you to remain in Ephesus—I going on to Macedonia—that you might charge certain [ones] not to teach any other thing,
4 wala wasitoe muda wao kwa hadithi za kubuniwa na orodha za majina ya vizazi visivyo na mwisho, ambazo huchochea mabishano badala ya mpango wa Mungu utokanao na imani.
nor to give heed to fables and endless genealogies, that cause questions rather than [the] stewardship of God which [is] in faith.
5 Kusudi la maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli.
And the end of the charge is love out of a pure heart, and of a good conscience, and of unhypocritical faith,
6 Watu wengine wamepotoka kutoka haya na kugeukia majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa,
from which certain [men], having swerved, turned aside to vain discourse,
7 wanataka kuwa walimu wa sheria, lakini hawajui mambo yale wanayosema wala hayo wanayoyatumainia kwa uthabiti.
willing to be teachers of law, not understanding either the things they say, nor concerning what they confidently assert,
8 Tunajua kwamba sheria ni njema ikiwa inatumika kwa halali kama ilivyokusudiwa.
and we have known that the Law [is] good, if anyone may use it lawfully;
9 Lakini tunajua ya kuwa sheria si kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, kwa ajili ya wasiomcha Mungu na wenye dhambi, wasio watakatifu na wanaokufuru; kwa wale wawauao baba zao au mama zao, kwa wauaji,
having known this, that law is not set for a righteous man, but for lawless and insubordinate persons, ungodly and sinners, impious and profane, murderers of fathers and murderers of mothers, manslayers,
10 kwa wazinzi na wahanithi, kwa wale wauzao watu, na kwa waongo na waapao kwa uongo, na kwa chochote kingine kilicho kinyume na mafundisho ya kweli,
whoremongers, homosexuals, enslavers, liars, perjured persons, and if there be any other thing that is adverse to sound doctrine,
11 ambayo yanakubaliana na Injili ya utukufu wa Mungu anayehimidiwa, ambayo mimi nimewekewa amana.
according to the good news of the glory of the blessed God, with which I was entrusted.
12 Namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa sababu aliniona mwaminifu, akaniteua kwa kazi yake.
And I give thanks to Him who enabled me—Christ Jesus our Lord—that He reckoned me steadfast, having put [me] to the ministry,
13 Ingawa wakati fulani nilikuwa mwenye kukufuru, mtesaji na mwenye jeuri, lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda hivyo kwa kutojua na kutoamini kwangu.
who before was speaking slander, and persecuting, and insulting, but I found kindness, because, being ignorant, I did [it] in unbelief,
14 Neema ya Bwana wetu ilimiminwa juu yangu kwa wingi, ikiambatana na imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.
and the grace of our Lord exceedingly abounded, with faith and love that [is] in Christ Jesus.
15 Msemo huu ni wa kweli na unaostahili kukubalika, usemao kwamba: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi, ambao mimi ndiye niliye mbaya kuliko wote.
The word [is] steadfast, and worthy of all acceptance, that Christ Jesus came into the world to save sinners—of whom I am first;
16 Lakini kwa sababu hiyo nilipata rehema, ili katika mimi, niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo Yesu apate kuonyesha uvumilivu wake usio na kikomo, ili niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini na wapate uzima wa milele. (aiōnios g166)
but because of this I found kindness, that Jesus Christ might first show forth all long-suffering in me, for a pattern of those about to believe on Him to continuous life. (aiōnios g166)
17 Basi Mfalme wa milele, asiye na mwisho, asiyeonekana, aliye Mungu pekee, apewe heshima na utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
And to the King of the ages, the incorruptible, invisible, only wise God, [is] honor and glory through the ages of the ages! Amen. (aiōn g165)
18 Mwanangu Timotheo, ninakupa agizo hili, kwa kadiri ya maneno ya unabii yaliyosemwa kukuhusu, ili kwa kuyafuata upate kupigana vita vizuri,
I commit to you this charge, child Timotheus, according to the prophecies that went before on you, that you may war in them the good warfare,
19 ukiishikilia imani na dhamiri njema, ambazo wengine wamevikataa, na hivyo wakaangamia kwa habari ya imani yao.
having faith and a good conscience, which some having thrust away, made shipwreck concerning the faith,
20 Miongoni mwao wako Himenayo na Aleksanda, ambao nimemkabidhi Shetani ili wafundishwe wasije wakakufuru.
of whom are Hymenaeus and Alexander, whom I delivered to Satan, that they might be instructed not to speak evil.

< 1 Timotheo 1 >