< 1 Timotheo 5 >
1 Usimkemee mzee kwa ukali bali umshawishi kama vile angekuwa ni baba yako. Uwatendee vijana kama vile ndugu zako;
Starszego [człowieka] nie strofuj, lecz nakłaniaj jak ojca, młodszych – jak braci;
2 nao wanawake wazee uwatendee kama mama zako, na wanawake vijana kama dada zako, katika usafi wote.
Starsze kobiety – jak matki, młodsze – jak siostry, z całą czystością.
3 Waheshimu wanawake wajane ambao ni wajane kweli kweli.
Okazuj szacunek wdowom, które rzeczywiście [są] wdowami.
4 Kama mjane ana watoto ama wajukuu, hawa inawapasa awali ya yote wajifunze kutimiza wajibu wao wa kumcha Mungu katika matendo kwa kuwatunza wale wa jamaa zao wenyewe, na hivyo wawarudishie wema waliowatendea wazazi wao, kwa kuwa hivi ndivyo impendezavyo Mungu.
Jeśli zaś jakaś wdowa ma dzieci lub wnuki, niech się one najpierw uczą być pobożnymi względem własnego domu i odwzajemniać się rodzicom; jest to bowiem [rzecz] dobra i miła w oczach Boga.
5 Mwanamke ambaye ni mjane kweli kweli, yaani, yeye aliyebaki peke yake huweka tumaini lake kwa Mungu naye hudumu katika maombi usiku na mchana akimwomba Mungu ili amsaidie.
Ta zaś, która rzeczywiście jest wdową i [jest] osamotniona, pokłada nadzieję w Bogu i trwa w prośbach i modlitwach we dnie i w nocy.
6 Lakini mjane aishiye kwa anasa amekufa, ingawa anaishi.
Lecz ta, która oddaje się rozkoszom, jest martwa, chociaż żyje.
7 Wape watu maagizo haya pia, ili asiwepo yeyote wa kulaumiwa.
To więc nakazuj, żeby były nienaganne.
8 Kama mtu hawatunzi wale wa jamaa yake, hasa wale wa nyumbani mwake mwenyewe, ameikana imani, tena ni mbaya kuliko yeye asiyeamini.
A jeśli ktoś nie dba o swoich, a zwłaszcza o domowników, ten wyparł się wiary i gorszy jest od niewierzącego.
9 Mjane yeyote asiwekwe kwenye orodha ya wajane isipokuwa awe ametimiza umri wa miaka sitini, na ambaye alikuwa mke wa mume mmoja,
Do wdów niech będzie zaliczona taka, która nie ma mniej niż sześćdziesiąt lat, była żoną jednego męża;
10 awe ameshuhudiwa kwa matendo yake mema, aliyewalea watoto wake vizuri, aliye mkarimu, aliyewanawisha watakatifu miguu, aliyewasaidia wenye shida na aliyejitolea kwa ajili ya matendo mema ya kila namna.
Znana z dobrych uczynków, jeśli wychowała dzieci, jeśli udzielała gościny, jeśli obmywała nogi świętym, jeśli wspomagała strapionych, jeśli wykonywała każdy dobry uczynek.
11 Lakini kwa habari za wajane vijana usiwaweke kwenye orodha hiyo, maana tamaa zao za kimaumbile zikizidi kule kujitoa kwao kwa Kristo, watataka kuolewa tena.
Natomiast młodszych wdów [do nich] nie zaliczaj, bo gdy rozkosze odwodzą je od Chrystusa, chcą wyjść za mąż;
12 Nao kwa njia hiyo watajiletea hukumu kwa kukiuka ahadi yao ya kwanza.
Ściągając na siebie potępienie, ponieważ odrzuciły pierwszą wiarę.
13 Zaidi ya hayo, wajane kama hao huwa na tabia ya uvivu wakizurura nyumba kwa nyumba, wala hawawi wavivu tu, bali pia huwa wasengenyaji, wajiingizao katika mambo yasiyowahusu na kusema mambo yasiyowapasa kusema.
Co więcej, uczą się bezczynności, chodząc od domu do domu, i nie tylko [są] bezczynne, lecz też gadatliwe, wścibskie, mówiące to, co nie wypada.
14 Hivyo nawashauri wajane vijana waolewe, wazae watoto na wasimamie nyumba zao, wasije wakampa adui nafasi ya kutushutumu.
Chcę więc, żeby młodsze wychodziły za mąż, rodziły dzieci, zajmowały się [domem], nie dawały przeciwnikowi żadnego powodu do obmowy.
15 Kwa maana kwa kweli wajane wengine wamepotoka ili kumfuata Shetani.
Już bowiem niektóre odwróciły się [i poszły] za szatanem.
16 Lakini kama mwanamke yeyote aaminiye ana wajane katika jamaa yake, inampasa awasaidie wala si kuwaacha wakililemea kanisa, ili kanisa liweze kuwasaidia wale ambao ni wajane kweli kweli.
[A] jeśli jakiś wierzący lub wierząca ma [w rodzinie] wdowy, niech im pomaga, aby kościół nie był obciążony i mógł przyjść z pomocą tym, które rzeczywiście są wdowami.
17 Wazee wa kanisa wanaoongoza shughuli za kanisa vizuri wanastahili heshima mara mbili, hasa wale ambao kazi yao ni kuhubiri na kufundisha.
Starsi, którzy dobrze przewodzą, niech będą uważani za godnych podwójnej czci, [a] zwłaszcza ci, którzy pracują w słowie i w nauce.
18 Kwa maana Maandiko husema, “Usimfunge maksai kinywa apurapo nafaka,” tena, “Mfanyakazi anastahili mshahara wake.”
Mówi bowiem Pismo: Młócącemu wołowi nie zawiążesz pyska, oraz: Godny jest robotnik swojej zapłaty.
19 Usiendekeze mashtaka dhidi ya mzee isipokuwa yawe yameletwa na mashahidi wawili au watatu.
Nie przyjmuj oskarżenia przeciwko starszemu, chyba że na podstawie [zeznania] dwóch albo trzech świadków.
20 Wale wanaodumu katika dhambi uwakemee hadharani, ili wengine wapate kuogopa.
A tych, którzy grzeszą, strofuj w obecności wszystkich, aby i inni się bali.
21 Ninakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu na mbele za malaika wateule, shika maagizo haya pasipo ubaguzi wala upendeleo.
Zaklinam [cię] wobec Boga i Pana Jezusa Chrystusa, i wybranych aniołów, abyś tego przestrzegał, nie mając względu na osoby, nie kierując się stronniczością.
22 Usiwe na haraka kumwekea mtu mikono wala usishiriki dhambi za watu wengine. Jilinde nafsi yako uwe safi.
Rąk na nikogo pospiesznie nie wkładaj ani nie bądź uczestnikiem cudzych grzechów. Siebie samego zachowaj czystym.
23 Acha kunywa maji peke yake, tumia divai kidogo kwa sababu ya tumbo lako na maumivu yako ya mara kwa mara.
[Samej] wody już nie pij, ale używaj trochę wina ze względu na twój żołądek i częste niedomagania.
24 Dhambi za watu wengine ni dhahiri nazo zinawatangulia kwenda hukumuni; na dhambi za watu wengine zinawafuata nyuma yao.
Grzechy niektórych ludzi są jawne, [jeszcze] zanim zostaną osądzone, a za niektórymi idą w ślad.
25 Vivyo hivyo, matendo mema yako dhahiri, na hata yale ambayo si mema hayawezi kufichika.
Podobnie dobre uczynki są jawne, a te, które nie są, pozostać w ukryciu nie mogą.