< 1 Timotheo 4 >

1 Roho asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
Mas o Espírito diz expressamente que nos últimos tempos alguns se afastarão da fé, dando atenção a espíritos enganadores, e a doutrinas de demônios,
2 Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.
por meio da hipocrisia de mentirosos, que têm a sua própria consciência cauterizada.
3 Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
Eles proibirão o casamento, e [mandarão] se abster dos alimentos que Deus criou para que sejam usados com gratidão pelos fiéis e pelos que conheceram a verdade.
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,
Pois toda criatura de Deus é boa, e não há nada a rejeitar, se for recebida com gratidão.
5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
Porque ela é santificada pela palavra de Deus e [pela] oração.
6 Kama ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.
Se informares essas coisas aos irmãos, serás um bom servidor de Cristo Jesus, alimentado com as palavras da fé e de boa doutrina que tens seguido.
7 Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.
Mas rejeita os mitos profanos e de velhas, e exercita-te na devoção divina.
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.
Pois o exercício do corpo tem pouco proveito; mas a devoção divina é proveitosa para tudo, pois tem as promessas da vida atual e da futura.
9 Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa,
[Esta] palavra é fiel, e digna de toda aceitação.
10 (nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi), kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
Pois para isto trabalhamos e lutamos, porque esperamos o Deus vivo, que é o Salvador de todos, especialmente dos crentes.
11 Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
Manda essas coisas, e ensina.
12 Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
Ninguém despreze a tua juventude, mas sê exemplo aos crentes, na palavra, no comportamento, no amor, na fé, e na pureza.
13 Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
Persiste na leitura, na exortação e no ensino, até que eu venha.
14 Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
Não desprezes o dom que está em ti, que te foi dado por profecia, com a imposição das mãos dos presbíteros.
15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
Medita nessas coisas, e nelas te ocupe, para que o teu progresso seja visível por todos.
16 Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
Tem cuidado de ti mesmo e da doutrina; persevera nessas coisas; porque, se fizeres isso, salvarás tanto a ti mesmo como aos que te ouvem.

< 1 Timotheo 4 >