< 1 Timotheo 4 >
1 Roho asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
But the Spirit says expressly that in later times some will fall away from the faith, paying attention to seducing spirits and doctrines of demons,
2 Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.
through the hypocrisy of men who speak lies, branded in their own conscience as with a hot iron,
3 Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
forbidding marriage and commanding to abstain from foods which God created to be received with thanksgiving by those who believe and know the truth.
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,
For every creature of God is good, and nothing is to be rejected if it is received with thanksgiving.
5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
For it is sanctified through the word of God and prayer.
6 Kama ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.
If you instruct the brothers of these things, you will be a good servant of Messiah Yeshua, nourished in the words of the faith and of the good doctrine which you have followed.
7 Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.
But refuse profane and old wives’ fables. Exercise yourself toward godliness.
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.
For bodily exercise has some value, but godliness has value in all things, having the promise of the life which is now and of that which is to come.
9 Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa,
This saying is faithful and worthy of all acceptance.
10 (nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi), kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
For to this end we both labor and suffer reproach, because we have set our trust in the living God, who is the Savior of all men, especially of those who believe.
11 Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
Command and teach these things.
12 Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
Let no man despise your youth; but be an example to those who believe, in word, in your way of life, in love, in spirit, in faith, and in purity.
13 Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
Until I come, pay attention to reading, to exhortation, and to teaching.
14 Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
Don’t neglect the gift that is in you, which was given to you by prophecy with the laying on of the hands of the elders.
15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
Be diligent in these things. Give yourself wholly to them, that your progress may be revealed to all.
16 Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
Pay attention to yourself and to your teaching. Continue in these things, for in doing this you will save both yourself and those who hear you.