< 1 Timotheo 4 >
1 Roho asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
Now the Spirit saith expressly, that in the latter times some will depart from the faith, giving heed to seducing spirits and teachings of demons,
2 Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.
through the hypocrisy of speakers of lies, who bear a brand on their own conscience,
3 Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
forbidding to marry, and commanding to abstain from food which God created to be received with thanksgiving, for those who believe and know the truth.
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,
For every creature of God is good, and nothing to be refused, if it be received with thanksgiving;
5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
for it is sanctified by the word of God and prayer.
6 Kama ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.
If thou lay these things before the brethren, thou wilt be a good minister of Christ Jesus, nourished in the words of the faith, and of the good teaching, with which thou art well acquainted.
7 Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.
But avoid the profane and old wives' fables; and exercise thyself unto godliness.
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.
For bodily exercise is profitable for little; but godliness is profitable for all things, having promise of the life that now is, and of that which is to come.
9 Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa,
True is the saying, and worthy of all acceptance.
10 (nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi), kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
For to this end we both labor and suffer reproach, because we have placed our hope in the living God, who is the Saviour of all men, especially of believers.
11 Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
These things command and teach.
12 Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
Let no one despise thy youth, but become an example to the believers, in word, in behavior, in love, in faith, in purity.
13 Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
Till I come, give attention to reading, to exhortation, to teaching.
14 Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
Neglect not the gift that is in thee, which was given thee by prophecy, with the laying on of the hands of the presbytery.
15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
Meditate on these things, give thyself wholly to them; that thy progress may be manifest to all.
16 Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
Give heed to thyself, and to thy teaching; continue in them; for in doing this thou wilt save both thyself and them that hear thee.