< 1 Timotheo 4 >
1 Roho asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
Duh izričito govori da će u posljednja vremena neki otpasti od vjere i prikloniti se prijevarnim duhovima i zloduhovskim naucima.
2 Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.
A sve to pod utjecajem himbe lažljivaca otupjele savjesti
3 Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
koji zabranjuju ženiti se i nameću uzdržavati se od jela što ih je Bog stvorio da ih sa zahvalnošću uzimaju oni koji vjeruju i znaju istinu.
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,
Doista, svako je Božje stvorenje dobro i ne valja odbaciti ništa što se uzima sa zahvalnošću
5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
jer se posvećuje riječju Božjom i molitvom.
6 Kama ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.
To izlaži braći i bit ćeš dobar poslužitelj Krista Isusa, hranjen riječima vjere i dobroga nauka za kojim postojano ideš.
7 Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.
Svjetovne pak i bablje priče odbijaj! Vježbaj se u pobožnosti!
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.
Uistinu, tjelesno vježbanje malo čemu koristi, a pobožnost je svemu korisna jer joj je obećan život - sadašnji i budući.
9 Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa,
Vjerodostojna je to riječ i vrijedna da se posve prihvati.
10 (nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi), kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
Ta za to se trudimo i borimo jer se pouzdajemo u Boga živoga koji je Spasitelj svih ljudi, ponajpače vjernika.
11 Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
Zapovijedaj to i naučavaj!
12 Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
Nitko neka ne prezire tvoje mladosti, nego budi uzor vjernicima u riječi, u vladanju, u ljubavi, u vjeri, u čistoći.
13 Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
Dok ne dođem, posveti se čitanju, poticanju, poučavanju.
14 Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
Ne zanemari milosnog dara koji je u tebi, koji ti je dan po proroštvu zajedno s polaganjem ruku starješinstva.
15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
Oko toga nastoj, sav u tom budi da tvoj napredak bude svima očit.
16 Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
Pripazi na samog sebe i na poučavanje! Ustraj u tome! Jer to vršeći, spasit ćeš i sebe i one koji te slušaju.