< 1 Timotheo 4 >

1 Roho asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
ܪܘܚܐ ܕܝܢ ܦܫܝܩܐܝܬ ܐܡܪܐ ܕܒܙܒܢܐ ܐܚܪܝܐ ܢܦܪܩܘܢ ܐܢܫ ܐܢܫ ܡܢ ܗܝܡܢܘܬܐ ܘܢܐܙܠܘܢ ܒܬܪ ܪܘܚܐ ܛܥܝܬܐ ܘܒܬܪ ܝܘܠܦܢܐ ܕܫܐܕܐ
2 Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.
ܗܠܝܢ ܕܒܐܤܟܡܐ ܕܓܠܐ ܡܛܥܝܢ ܘܡܡܠܠܝܢ ܟܕܒܘܬܐ ܘܟܘܝܢ ܒܬܐܪܬܗܘܢ
3 Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
ܘܟܠܝܢ ܠܡܙܕܘܓܘ ܘܡܦܪܩܝܢ ܡܢ ܡܐܟܠܬܐ ܐܝܠܝܢ ܕܐܠܗܐ ܒܪܐ ܐܢܝܢ ܠܚܘܫܚܐ ܘܠܬܘܕܝܬܐ ܠܐܝܠܝܢ ܕܡܗܝܡܢܝܢ ܘܝܕܥܝܢ ܫܪܪܐ
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,
ܡܛܠ ܕܟܠ ܕܒܪܐ ܠܐܠܗܐ ܫܦܝܪ ܗܘ ܘܠܝܬ ܡܕܡ ܕܡܤܠܝ ܐܢ ܒܬܘܕܝܬܐ ܢܬܢܤܒ
5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
ܡܬܩܕܫ ܓܝܪ ܒܡܠܬܐ ܕܐܠܗܐ ܘܒܨܠܘܬܐ
6 Kama ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.
ܗܠܝܢ ܐܢ ܬܗܘܐ ܡܠܦ ܠܐܚܝܟ ܡܫܡܫܢܐ ܛܒܐ ܬܗܘܐ ܕܝܫܘܥ ܡܫܝܚܐ ܟܕ ܡܬܪܒܐ ܐܢܬ ܒܡܠܐ ܕܗܝܡܢܘܬܐ ܘܒܝܘܠܦܢܐ ܛܒܐ ܕܝܠܝܦ ܐܢܬ
7 Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.
ܡܢ ܫܘܥܝܬܐ ܕܝܢ ܦܟܝܗܬܐ ܕܤܒܬܐ ܐܫܬܐܠ ܘܕܪܫ ܢܦܫܟ ܒܟܐܢܘܬܐ
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.
ܕܘܪܫܐ ܓܝܪ ܕܦܓܪܐ ܙܒܢܐ ܗܘ ܙܥܘܪܐ ܡܘܬܪ ܟܐܢܘܬܐ ܕܝܢ ܒܟܠ ܡܕܡ ܡܘܬܪܐ ܘܐܝܬ ܠܗ ܫܘܘܕܝܐ ܕܚܝܐ ܕܙܒܢܐ ܗܢܐ ܘܕܥܬܝܕ
9 Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa,
ܡܗܝܡܢܐ ܗܝ ܡܠܬܐ ܘܫܘܝܐ ܗܝ ܠܡܩܒܠܘܬܗ
10 (nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi), kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
ܡܛܠ ܗܕܐ ܗܘ ܓܝܪ ܠܐܝܢܢ ܘܡܬܚܤܕܝܢܢ ܕܡܤܒܪܝܢܢ ܒܐܠܗܐ ܚܝܐ ܕܐܝܬܘܗܝ ܡܚܝܢܐ ܕܒܢܝܢܫܐ ܟܠܗܘܢ ܝܬܝܪܐܝܬ ܕܡܗܝܡܢܐ
11 Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
ܗܠܝܢ ܐܠܦ ܘܦܩܕ
12 Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
ܘܠܐ ܐܢܫ ܢܒܤܐ ܥܠ ܛܠܝܘܬܟ ܐܠܐ ܗܘܝ ܕܡܘܬܐ ܠܡܗܝܡܢܐ ܒܡܠܬܐ ܘܒܗܘܦܟܐ ܘܒܚܘܒܐ ܘܒܗܝܡܢܘܬܐ ܘܒܕܟܝܘܬܐ
13 Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
ܥܕ ܐܬܐ ܐܢܐ ܐܬܚܦܛ ܒܩܪܝܢܐ ܘܒܒܥܘܬܐ ܘܒܝܘܠܦܢܐ
14 Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
ܘܠܐ ܬܒܤܐ ܒܡܘܗܒܬܐ ܕܐܝܬ ܒܟ ܗܝ ܕܐܬܝܗܒܬ ܠܟ ܒܢܒܝܘܬܐ ܘܒܤܝܡ ܐܝܕܐ ܕܩܫܝܫܘܬܐ
15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
ܒܗܠܝܢ ܐܬܗܓܐ ܘܒܗܝܢ ܗܘܝ ܕܬܬܝܕܥ ܠܟܠܢܫ ܕܠܩܕܡܝܟ ܐܬܐ ܐܢܬ
16 Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
ܘܐܙܕܗܪ ܒܢܦܫܟ ܘܒܝܘܠܦܢܟ ܘܚܡܤܢ ܒܗܘܢ ܟܕ ܗܠܝܢ ܓܝܪ ܬܥܒܕ ܢܦܫܟ ܬܚܐ ܘܠܐܝܠܝܢ ܕܫܡܥܝܢ ܠܟ

< 1 Timotheo 4 >