< 1 Timotheo 3 >
1 Hili ni neno la kuaminiwa, kwamba mtu akitamani kazi ya uangalizi, atamani kazi nzuri.
Истинита је реч: ако ко владичанство жели добру ствар жели.
2 Basi, imempasa mwangalizi awe mtu asiye na lawama, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, anayejitawala, anayeheshimika, mkarimu, ajuaye kufundisha,
Али владика треба да је без мане, једне жене муж, трезан, паметан, поштен, гостољубив, вредан да учи;
3 asiwe mlevi, wala mkali bali awe mpole, asiwe mgomvi wala mpenda fedha.
Не пијаница, не бојац, не лаком, него кротак, миран, не среброљубац;
4 Lazima aweze kuisimamia nyumba yake mwenyewe vizuri na kuhakikisha kwamba watoto wake wanamtii na kuwa na heshima kwa kila njia.
Који својим домом добро управља, који има послушну децу са сваким поштењем;
5 (Kwa maana kama mtu hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atawezaje kuliangalia kanisa la Mungu?)
А ако ко не уме својим домом управљати, како ће се моћи старати за цркву Божију?
6 Asiwe mtu aliyeokoka karibuni asije akajivuna na kuangukia kwenye hukumu ile ile ya ibilisi.
Не новокрштен, да се не би надуо, и упао у суд ђавољи.
7 Inampasa pia awe na sifa njema kwa watu walio nje, ili asije akalaumiwa na kuanguka kwenye mtego wa ibilisi.
А ваља да има и добро сведочанство од оних који су напољу, да не би упао у срамоту и у замку ђавољу.
8 Vivyo hivyo, mashemasi nao wawe watu wanaostahili heshima, wasiwe wenye kauli mbili au wenye kujifurahisha kwa mvinyo, wala wanaotamani faida isiyo halali.
Тако и ђакони треба да буду поштени, не двојезични, не који много вина пију, не лакоми на добитак поган,
9 Inawapasa kushikamana sana na ile siri ya imani kwa dhamiri safi.
Који имају тајну вере у чистој савести.
10 Ni lazima wapimwe kwanza; kisha kama hakuna neno dhidi yao, basi na waruhusiwe kuhudumu kama mashemasi.
А и ови да се кушају најпре, па онда да служе, ако су без мане.
11 Vivyo hivyo, wake zao wawe wanawake wanaostahili heshima, wasio wasingiziaji, bali wawe na kiasi na waaminifu katika kila jambo.
Тако и жене треба да су поштене, не које опадају, трезне, верне у свему.
12 Shemasi awe mume wa mke mmoja na inampasa aweze kusimamia watoto wake na watu wa nyumbani mwake vyema.
Ђакони да бивају јединих жена мужеви, који добро управљају децом и својим домовима.
13 Wale ambao wamehudumu vyema katika huduma ya ushemasi hujipatia msimamo bora na ujasiri mkubwa katika imani yao ndani ya Kristo Yesu.
Јер који добро служе они добијају себи добар поступ, и велику слободу у вери Исуса Христа.
14 Ingawa ninatarajia kuja kwako hivi karibuni, ninakuandikia maagizo haya sasa ili kwamba,
Ово ти пишем надајући се да ћу скоро доћи к теби.
15 kama nikikawia, utajua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, ambayo ndiyo kanisa la Mungu aliye hai, lililo nguzo na msingi wa kweli.
Ако ли се забавим, да знаш како треба живети у дому Божијем, који је црква Бога Живога, ступ и тврђа истине.
16 Bila shaka yoyote, siri ya utauwa ni kubwa: Alidhihirishwa katika mwili wa kibinadamu, akathibitishwa kuwa na haki katika Roho, akaonekana na malaika, akahubiriwa miongoni mwa mataifa, akaaminiwa ulimwenguni, akachukuliwa juu katika utukufu.
И, као што је признато, велика је тајна побожности: Бог се јави у телу, оправда се у Духу, показа се анђелима, проповеди се незнабошцима, верова се на свету, узнесе се у слави.