< 1 Timotheo 2 >

1 Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
Je recommande donc, avant toutes choses, qu'on fasse des requêtes, des prières, des supplications et des actions de grâces pour tous les hommes,
2 kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
pour les rois et pour tous ceux qui exercent l'autorité, afin que nous puissions mener une vie paisible et tranquille, en toute piété et en toute honnêteté.
3 Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
C'est là une chose bonne et agréable aux yeux de Dieu, notre Sauveur,
4 anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
qui veut que tous les hommes soient sauvés et parviennent à la connaissance de la vérité.
5 Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
En effet, il y a un seul Dieu, et un seul Médiateur entre Dieu et les hommes, Jésus-Christ, homme,
6 aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
qui s'est donné lui-même en rançon pour tous. Tel est le témoignage qui a été rendu en son temps,
7 Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
et pour lequel — je dis la vérité, je ne mens point. — j'ai été établi prédicateur, apôtre et docteur des Païens, afin de les instruire dans la foi et dans la vérité.
8 Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
Je veux donc que les hommes prient en tout lieu, élevant au ciel des mains pures, sans colère et sans contestation.
9 Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
Je veux aussi que les femmes s'habillent d'une manière décente, qu'avec pudeur et modestie elles se parent, non de tresses ou d'or, de perles ou de vêtements somptueux,
10 bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
mais de bonnes oeuvres, comme il convient à des femmes qui font profession de piété.
11 Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
Que la femme écoute l'instruction en silence, avec une entière soumission.
12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
Je ne permets pas à la femme d'enseigner, ni de prendre autorité sur l'homme; mais elle doit demeurer dans le silence.
13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
Car Adam fut formé le premier, et Eve ensuite.
14 Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
Et ce n'est pas Adam qui fut séduit; mais la femme, ayant été séduite, tomba dans la transgression.
15 Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.
Cependant, elle sera sauvée en devenant mère, si elle persévère sagement dans la foi, dans la charité et dans la sanctification.

< 1 Timotheo 2 >