< 1 Timotheo 2 >
1 Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
J'exhorte donc qu'avant toutes choses on fasse des requêtes, des prières, des supplications, et des actions de grâces pour tous les hommes;
2 kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
Pour les Rois, et pour tous ceux qui sont constitués en dignité, afin que nous puissions mener une vie paisible et tranquille, en toute piété et honnêteté.
3 Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
Car cela est bon et agréable devant Dieu notre Sauveur;
4 anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
Qui veut que tous les hommes soient sauvés, et qu'ils viennent à la connaissance de la vérité.
5 Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
Car il y a un seul Dieu, et un seul Médiateur entre Dieu et les hommes, [savoir] Jésus-Christ homme;
6 aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
Qui s'est donné soi-même en rançon pour tous, témoignage qui a été rendu en son temps.
7 Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
C'est dans cette vue que j'ai été établi Prédicateur, Apôtre ( je dis la vérité en Christ, je ne mens point), et Docteur des Gentils en la foi, et en la vérité.
8 Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
Je veux donc que les hommes prient en tout lieu, levant leurs mains pures, sans colère, et sans dispute.
9 Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
Que les femmes aussi se parent d'un vêtement honnête, avec pudeur et modestie, non point avec des tresses ni avec de l'or, ni des perles, ni des habillements somptueux;
10 bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
Mais [qu'elles soient] ornées de bonnes œuvres, comme il est séant à des femmes qui font profession de servir Dieu.
11 Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
Que la femme apprenne dans le silence en toute soumission.
12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
Car je ne permets point à la femme d'enseigner, ni d'user d'autorité sur le mari; mais elle doit demeurer dans le silence.
13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
Car Adam a été formé le premier, et puis Eve.
14 Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
Et ce n'a point été Adam qui a été séduit, mais la femme ayant été séduite, a été la cause de la transgression.
15 Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.
Elle sera néanmoins sauvée en mettant des enfants au monde, pourvu qu'elle persévère dans la foi, dans la charité, et dans la sanctification, avec modestie.