< 1 Timotheo 2 >

1 Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
I REQUIRE then from thee, that, before every thing supplication be offered to Aloha, and prayer and intercession and thanksgiving for all men;
2 kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
for kings and princes, that an habitation quiet and tranquil we may inhabit in all the fear of Aloha and purity.
3 Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
For this is good and acceptable before Aloha our Saviour;
4 anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
who willeth that all men should be saved, and turn to the knowledge of the truth.
5 Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
For one is Aloha, and one is the Mediator of Aloha and of men; the man Jeshu Meshiha,
6 aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
who gave himself a ransom for every man; a testimony which cometh in its time,
7 Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
of which I am constituted an herald and an apostle, I say the truth and lie not, to be a teacher of the nations in the faith of the truth.
8 Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
I wish then for men to pray in every place, uplifting their hands purely and without wrath and without disputations.
9 Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
So also let women with decorous simplicity of apparel, with modesty and with chastity, adorn themselves, not with braidings, and with gold, and with pearls, and with fine vestments,
10 bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
but with good works, as becometh women who profess the fear of Aloha.
11 Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
Let the wife in quietude learn with all submission:
12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
for unto the wife to teach I permit not, neither to be authoritative over the husband, but to be in quietude.
13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
For Adam was formed first, then Hava;
14 Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
and Adam was not deceived, but the wife was deceived, and transgressed the commandment.
15 Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.
But she is saved by her children, if they continue in faith, and in love, and in sanctification, and in chastity.

< 1 Timotheo 2 >