< 1 Timotheo 2 >

1 Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
首先,我想鼓励你为每个人祈祷:请求上帝,代表他们提出要求,表示感谢。
2 kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
为君王和所有类型的领袖也这样祷告,让我们可以过上平静祥和的生活,时刻想着上帝,认真对待生活。
3 Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
我们的救主上帝会认为这是好事情,可让他喜悦。
4 anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
他希望所有人都得救,真正理解真理是什么。
5 Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
因为只有一个上帝,在上帝和人类之间只有一个中间人,那就是降生为人的基督耶稣。
6 aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
他舍弃自己,以使我们都能被赢回,在恰当的时间显示证据。
7 Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
我受到指派分享这个讯息,成为信使,教授异族人,让他们相信上帝和真理。
8 Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
我真正希望的是所有地方的男人都没有愤怒或争论,能够虔诚地向上帝祈祷。
9 Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
照样,女人应该端庄、适度、恰如其分地装扮,她们的美不应来自其发型、佩戴的黄金和珍珠珠宝或昂贵的服装,
10 bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
却要以善行为美,这才是愿意追随上帝的女性恰当的行为。
11 Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
女人应该学会保持安静,尊重她们所在的地位。
12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
我不允许女人成为引导者,或去控制男人;她们应该保持安静。
13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
因为先造了亚当,后造的夏娃;
14 Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
并非亚当受到欺骗,而是夏娃被彻底欺骗,在罪中堕落。
15 Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.
但女人仍然可以通过做母亲而获得救赎,只要他们始终保持信心、爱心、遵循圣洁而庄重的生活。。

< 1 Timotheo 2 >