< 1 Timotheo 1 >

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.
PAULOS, an apostle of Jeshu Meshiha, by the commandment of Aloha our Saviour, and of Jeshu Meshiha our hope;
2 Kwa Timotheo, mwanangu halisi katika imani: Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timotheos, my true son in the faith: grace and mercy and peace from Aloha our Father and Jeshu Meshiha our Lord.
3 Kama nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia, endelea kubaki Efeso, ili kwamba upate kuwaagiza watu wasiendelee kufundisha mafundisho ya uongo
I requested of thee, when I would go into Makedunia, to remain at Ephesos, and instruct certain men that they teach not various doctrines,
4 wala wasitoe muda wao kwa hadithi za kubuniwa na orodha za majina ya vizazi visivyo na mwisho, ambazo huchochea mabishano badala ya mpango wa Mungu utokanao na imani.
nor throw themselves (away) upon stories and tales of generations which have no end, (but) which rather subserve contentions, and not edification in the faith of Aloha.
5 Kusudi la maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli.
But the end of the commandment is love, from a pure heart, and from a good conscience, and from genuine faith.
6 Watu wengine wamepotoka kutoka haya na kugeukia majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa,
And from them that have erred, and have declined to vain words,
7 wanataka kuwa walimu wa sheria, lakini hawajui mambo yale wanayosema wala hayo wanayoyatumainia kwa uthabiti.
seeking to become teachers of the law, while they understand not what they speak, nor that concerning which they contend.
8 Tunajua kwamba sheria ni njema ikiwa inatumika kwa halali kama ilivyokusudiwa.
But we know that the law is good, if a man according to the law converse in it;
9 Lakini tunajua ya kuwa sheria si kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, kwa ajili ya wasiomcha Mungu na wenye dhambi, wasio watakatifu na wanaokufuru; kwa wale wawauao baba zao au mama zao, kwa wauaji,
knowing that against the righteous the law is not set, but against the evil, and rebels, and the wicked, and sinners, and the dishonest, and those who are not pure, and those who strike their fathers, and those who strike their mothers, and murderers,
10 kwa wazinzi na wahanithi, kwa wale wauzao watu, na kwa waongo na waapao kwa uongo, na kwa chochote kingine kilicho kinyume na mafundisho ya kweli,
and fornicators, and liers with men, and stealers of the free, and liars, and doers against an oath
11 ambayo yanakubaliana na Injili ya utukufu wa Mungu anayehimidiwa, ambayo mimi nimewekewa amana.
and whatever (else) is opposed to the healthful doctrine of the gospel of the glory of the blessed Aloha, with which I have been intrusted.
12 Namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa sababu aliniona mwaminifu, akaniteua kwa kazi yake.
And I thank him who hath empowered me, our Lord Jeshu Meshiha, who accounted me faithful, and constituted me his minister; me,
13 Ingawa wakati fulani nilikuwa mwenye kukufuru, mtesaji na mwenye jeuri, lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda hivyo kwa kutojua na kutoamini kwangu.
who before was a blasphemer, and a persecutor, and injurious; but I received mercy, because while ignorant I did it, without faith.
14 Neema ya Bwana wetu ilimiminwa juu yangu kwa wingi, ikiambatana na imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.
But in me hath abounded the grace of our Lord, and faith and love which are in Jeshu Meshiha.
15 Msemo huu ni wa kweli na unaostahili kukubalika, usemao kwamba: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi, ambao mimi ndiye niliye mbaya kuliko wote.
Faithful is the word, and worthy of reception that Jeshu the Meshiha came into the world to save sinners, of whom I am first.
16 Lakini kwa sababu hiyo nilipata rehema, ili katika mimi, niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo Yesu apate kuonyesha uvumilivu wake usio na kikomo, ili niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini na wapate uzima wa milele. (aiōnios g166)
But for this he had compassion upon me, that in me first Jeshu Meshiha might show all long-suffering, as an exhibition for them who should believe in him unto everlasting life. (aiōnios g166)
17 Basi Mfalme wa milele, asiye na mwisho, asiyeonekana, aliye Mungu pekee, apewe heshima na utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
But to the King who is eternal, incorruptible, and unseen, who is one Aloha, be honour and glory for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
18 Mwanangu Timotheo, ninakupa agizo hili, kwa kadiri ya maneno ya unabii yaliyosemwa kukuhusu, ili kwa kuyafuata upate kupigana vita vizuri,
This commandment I commit to thee, my son Timotheos, according to the early prophecies which were concerning thee, that thou mayest war through them this good warfare with faith and with a good conscience.
19 ukiishikilia imani na dhamiri njema, ambazo wengine wamevikataa, na hivyo wakaangamia kwa habari ya imani yao.
For those who this have put away from them of faith have been emptied;
20 Miongoni mwao wako Himenayo na Aleksanda, ambao nimemkabidhi Shetani ili wafundishwe wasije wakakufuru.
as Hymeneos and Alexandros, whom I have delivered to Satana, that they may not blaspheme.

< 1 Timotheo 1 >