< 1 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike, ninyi mlio ndani ya Mungu Baba yetu na ndani ya Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na amani.
Pavel in Silván ter Timótej cerkvi Tesaloníčanov, ki je v Bogu Očetu in v Gospodu Jezusu Kristusu: ›Milost bodi vam in mir od Boga, našega Očeta in Gospoda Jezusa Kristusa.‹
2 Siku zote tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu ninyi nyote, tukiwataja kwenye maombi yetu daima.
Vedno se za vas vse zahvaljujemo Bogu in vas omenjamo v svojih molitvah,
3 Tunaikumbuka daima kazi yenu ya imani mbele za Mungu aliye Baba yetu, taabu yenu katika upendo na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo.
ko se brez prenehanja spominjamo vašega dela vere in truda ljubezni ter potrpežljivosti upanja v našega Gospoda Jezusa Kristusa, pred očmi Boga in našega Očeta;
4 Ndugu zetu mpendwao na Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba Mungu amewachagua,
ker poznamo, ljubljeni bratje, vašo izvolitev od Boga.
5 kwa sababu ujumbe wetu wa Injili haukuja kwenu kwa maneno matupu bali pia ulidhihirishwa katika nguvu na katika Roho Mtakatifu, tena ukiwa na uthibitisho kamili, kama vile ninyi wenyewe mnavyojua jinsi tulivyoenenda katikati yenu kwa ajili yenu.
Kajti naš evangelij ni prišel k vam samo v besedi, temveč tudi v moči in v Svetem Duhu in v precejšnjem zagotovilu; kakor veste, kakšne vrste ljudje smo bili med vami zaradi vas.
6 Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, ingawa mlipata mateso mengi, mlilipokea lile Neno kwa furaha katika Roho Mtakatifu.
In vi ste postali naši in Gospodovi sledilci, ker ste besedo sprejeli v veliki stiski, z veseljem Svetega Duha,
7 Hivyo ninyi mkawa kielelezo kwa waumini wote katika Makedonia na Akaya.
tako da ste bili zgledi vsem, ki verujejo v Makedoniji in Ahaji.
8 Kwa maana kutoka kwenu neno la Bwana limesikika, si katika Makedonia na Akaya tu, bali pia imani yenu katika Mungu imejulikana kila mahali kiasi kwamba hatuna haja ya kusema lolote kwa habari yake.
Kajti od vas je odmevala Gospodova beseda ne samo po Makedoniji in Ahaji, temveč se je vaša, do Boga usmerjena vera, razširila tudi naokoli, po vsakem kraju; tako da nam ni treba karkoli govoriti,
9 Kwa maana watu wa maeneo hayo wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli
kajti oni sami so o nas prikazali kakšne vrste prihod smo imeli k vam in kako ste se od malikov obrnili k Bogu, da služite živemu in resničnemu Bogu;
10 na ili kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu: yaani, Yesu, yeye aliyetuokoa kutoka ghadhabu inayokuja.
in da čakate na njegovega Sina iz nebes, ki ga je obudil od mrtvih, celó Jezusa, ki nas je osvobodil pred besom, ki pride.

< 1 Wathesalonike 1 >