< 1 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike, ninyi mlio ndani ya Mungu Baba yetu na ndani ya Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na amani.
Pavel a Silván a Timoteus církvi Tessalonicenských v Bohu Otci a Pánu Ježíši Kristu: Milost vám a pokoj od Boha Otce našeho a Pána Jezukrista.
2 Siku zote tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu ninyi nyote, tukiwataja kwenye maombi yetu daima.
Díky činíme Bohu vždycky ze všech vás, zmínku činíce o vás na modlitbách svých.
3 Tunaikumbuka daima kazi yenu ya imani mbele za Mungu aliye Baba yetu, taabu yenu katika upendo na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo.
Bez přestání pamatujíce na skutek víry vaší a na práci lásky, a na trpělivost naděje Pána našeho Jezukrista, před Bohem a Otcem naším,
4 Ndugu zetu mpendwao na Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba Mungu amewachagua,
Vědouce, bratří Bohu milí, o vyvolení vašem.
5 kwa sababu ujumbe wetu wa Injili haukuja kwenu kwa maneno matupu bali pia ulidhihirishwa katika nguvu na katika Roho Mtakatifu, tena ukiwa na uthibitisho kamili, kama vile ninyi wenyewe mnavyojua jinsi tulivyoenenda katikati yenu kwa ajili yenu.
Nebo evangelium naše k vám nezáleželo toliko v slovu, ale i v moci, i v Duchu svatém, a v jistotě mnohé, jakož víte, jací jsme byli mezi vámi pro vás.
6 Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, ingawa mlipata mateso mengi, mlilipokea lile Neno kwa furaha katika Roho Mtakatifu.
A vy následovníci naši i Páně učiněni jste, přijavše slovo ve mnohé úzkosti, s radostí Ducha svatého,
7 Hivyo ninyi mkawa kielelezo kwa waumini wote katika Makedonia na Akaya.
Tak že jste učiněni příklad všem věřícím v Macedonii a v Achaii.
8 Kwa maana kutoka kwenu neno la Bwana limesikika, si katika Makedonia na Akaya tu, bali pia imani yenu katika Mungu imejulikana kila mahali kiasi kwamba hatuna haja ya kusema lolote kwa habari yake.
Nebo od vás rozhlásilo se slovo Páně netoliko v Macedonii a v Achaii, ale i na všelikém místě víra vaše, kteráž jest v Boha, roznesla se, tak že nepotřebí nám o tom nic mluviti.
9 Kwa maana watu wa maeneo hayo wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli
Oniť zajisté sami o nás vypravují, jaký byl příchod náš k vám, a kterak jste se obrátili k Bohu od modl, abyste sloužili Bohu živému a pravému,
10 na ili kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu: yaani, Yesu, yeye aliyetuokoa kutoka ghadhabu inayokuja.
A očekávali Syna jeho s nebe, kteréhož vzkřísil z mrtvých, totiž Ježíše, kterýž vysvobodil nás od hněvu budoucího.

< 1 Wathesalonike 1 >