< 1 Wathesalonike 5 >

1 Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
Empero acerca de los tiempos y de los momentos, no tenéis, hermanos, necesidad de que yo os escriba:
2 kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
Porque vosotros sabéis perfectamente, que el día del Señor, como ladrón en la noche, así vendrá.
3 Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
Que cuando dirán: Paz y seguridad: entonces vendrá sobre ellos destrucción de repente, como los dolores del parto sobre la mujer preñada; y no escaparán.
4 Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
Mas vosotros, hermanos, no estáis en tinieblas, para que aquel día os agarre como ladrón.
5 Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
Porque todos vosotros sois hijos de la luz, e hijos del día: no somos hijos de la noche, ni hijos de las tinieblas.
6 Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
Así, pues, no durmamos como los demás; antes velemos y seamos sobrios.
7 Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
Porque los que duermen, de noche duermen; y los que están borrachos, de noche están borrachos.
8 Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
Mas nosotros, que somos hijos del día, seamos sobrios, vistiéndonos de la coraza de fe, y de amor, y por almete de la esperanza de salud.
9 Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Porque no nos ha puesto Dios para ira, sino para alcanzar salud por medio de nuestro Señor Jesu Cristo:
10 Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye.
El cual murió por nosotros; para que, o que velemos, o que durmamos, vivamos juntamente con él.
11 Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.
Por lo cual consoláos los unos a los otros, y edificáos uno a otro, así como lo hacéis.
12 Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
Y, os rogamos, hermanos, que reconozcáis a los que trabajan entre vosotros, y os presiden en el Señor, y os amonestan;
13 Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
Y que los tengáis en la mayor estima, amándolos a causa de su obra: tenéd paz entre vosotros mismos.
14 Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
Os exhortamos, pues, hermanos, que amonestéis a los que andan desordenadamente, que consoléis a los de poco ánimo, que soportéis a los flacos, que seáis sufridos para con todos.
15 Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
Mirád que ninguno dé a otro mal por mal; antes seguíd siempre lo bueno los unos para con los otros, y para con todos.
16 Furahini siku zote;
Estád siempre gozosos.
17 ombeni bila kukoma;
Orád sin cesar.
18 shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
En todo dad gracias; porque esta es la voluntad de Dios en Cristo Jesús acerca de vosotros.
19 Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
No apaguéis el Espíritu.
20 msiyadharau maneno ya unabii.
No menospreciéis las profecías.
21 Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
Examinádlo todo: retenéd lo que fuere bueno.
22 Jiepusheni na uovu wa kila namna.
Apartáos de toda apariencia de mal.
23 Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo.
Y el mismo Dios de paz os santifique cabalmente; y que todo vuestro espíritu, y alma y cuerpo sean guardados irreprensibles para la venida del Señor nuestro Jesu Cristo.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.
Fiel es el que os ha llamado, el cual también lo hará.
25 Ndugu, tuombeeni.
Hermanos, orád por nosotros.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Saludád a todos los hermanos con beso santo.
27 Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.
Conjúroos por el Señor, que esta carta sea leída a todos los santos hermanos.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.
La gracia de nuestro Señor Jesu Cristo sea con vosotros. Amén. La primera carta a los Tesalonicenses fue escrita de Aténas.

< 1 Wathesalonike 5 >