< 1 Wathesalonike 5 >
1 Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
De temporibus autem, et momentis fratres non indigetis ut scribamus vobis.
2 kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
Ipsi enim diligenter scitis quia dies Domini, sicut fur in nocte, ita veniet.
3 Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
cum enim dixerint pax, et securitas: tunc repentinus eis superveniet interitus, sicut dolor in utero habentis, et non effugient.
4 Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
Vos autem fratres non estis in tenebris, ut vos dies illa tamquam fur comprehendat:
5 Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
omnes enim vos filii lucis estis, et filii diei: non sumus noctis, neque tenebrarum.
6 Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
Igitur non dormiamus sicut et ceteri, sed vigilemus, et sobrii simus.
7 Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
Qui enim dormiunt, nocte dormiunt: et qui ebrii sunt, nocte ebrii sunt.
8 Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
Nos autem, qui diei sumus, sobrii simus, induti loricam fidei, et charitatis, et galeam spem salutis:
9 Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
quoniam non posuit nos Deus in iram, sed in acquisitionem salutis per Dominum nostrum Iesum Christum,
10 Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye.
qui mortuus est pro nobis: ut sive vigilemus, sive dormiamus, simul cum illo vivamus.
11 Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.
Propter quod consolamini invicem: et aedificate alterutrum, sicut et facitis.
12 Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
Rogamus autem vos fratres ut noveritis eos, qui laborant inter vos, et praesunt vobis in Domino, et monent vos,
13 Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
ut habeatis illos abundantius in charitate propter opus illorum: et pacem habete cum eis.
14 Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
Rogamus autem vos fratres, corripite inquietos, consolamini pusillanimes, suscipite infirmos, patientes estote ad omnes.
15 Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
Videte ne quis malum pro malo alicui reddat: sed semper quod bonum est sectamini in invicem, et in omnes.
Sine intermissione orate.
18 shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
In omnibus gratias agite: haec est enim voluntas Dei in Christo Iesu in omnibus vobis.
19 Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
Spiritum nolite extinguere.
20 msiyadharau maneno ya unabii.
Prophetias nolite spernere.
21 Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
Omnia autem probate: quod bonum est tenete.
22 Jiepusheni na uovu wa kila namna.
Ab omni specie mala abstinete vos:
23 Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo.
Ipse autem Deus pacis sanctificet vos per omnia: ut integer spiritus vester, et anima, et corpus sine querela in adventu Domini nostri Iesu Christi conservetur.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.
Fidelis est, qui vocavit vos: qui etiam faciet.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Salutate fratres omnes in osculo sancto.
27 Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.
Adiuro vos per Dominum ut legatur epistola haec omnibus sanctis fratribus.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.
Gratia Domini nostri Iesu Christi vobiscum. Amen.