< 1 Wathesalonike 5 >

1 Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
But concerning the times and the seasons, brothers, you have no need that anything be written to you.
2 kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
For you yourselves know well that the day of the Lord comes like a thief in the night.
3 Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
For when they are saying, “Peace and safety,” then sudden destruction will come on them, like birth pains on a pregnant woman. Then they will in no way escape.
4 Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
But you, brothers, aren’t in darkness, that the day should overtake you like a thief.
5 Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
You are all children of light and children of the day. We don’t belong to the night, nor to darkness,
6 Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
so then let’s not sleep, as the rest do, but let’s watch and be sober.
7 Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
For those who sleep, sleep in the night; and those who are drunk are drunk in the night.
8 Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
But since we belong to the day, let’s be sober, putting on the breastplate of faith and love, and for a helmet, the hope of salvation.
9 Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
For God didn’t appoint us to wrath, but to the obtaining of salvation through our Lord Jesus Christ,
10 Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye.
who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him.
11 Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.
Therefore exhort one another, and build each other up, even as you also do.
12 Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
But we beg you, brothers, to know those who labor among you, and are over you in the Lord and admonish you,
13 Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
and to respect and honor them in love for their work’s sake. Be at peace among yourselves.
14 Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
We exhort you, brothers: Admonish the disorderly; encourage the faint-hearted; support the weak; be patient toward all.
15 Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
See that no one returns evil for evil to anyone, but always follow after that which is good for one another and for all.
16 Furahini siku zote;
Always rejoice.
17 ombeni bila kukoma;
Pray without ceasing.
18 shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
In everything give thanks, for this is the will of God in Christ Jesus toward you.
19 Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
Don’t quench the Spirit.
20 msiyadharau maneno ya unabii.
Don’t despise prophecies.
21 Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
Test all things, and hold firmly that which is good.
22 Jiepusheni na uovu wa kila namna.
Abstain from every form of evil.
23 Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo.
May the God of peace himself sanctify you completely. May your whole spirit, soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.
He who calls you is faithful, who will also do it.
25 Ndugu, tuombeeni.
Brothers, pray for us.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Greet all the brothers with a holy kiss.
27 Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.
I solemnly command you by the Lord that this letter be read to all the holy brothers.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen.

< 1 Wathesalonike 5 >