< 1 Wathesalonike 5 >

1 Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
But of the times and the seasons, my brethren, you need not that I write to you;
2 kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
for you truly know that the day of our Lord as a thief in the night so cometh.
3 Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
While they shall be saying, Peace and tranquillity, then unawares will destruction arise against them, as distress upon the child-bearer, and they shall not escape.
4 Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
But you, my brethren, are not in darkness, that that day as a thief should overtake you.
5 Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
For all of you are sons of light, and sons of the day; and are not sons of the night, nor sons of darkness.
6 Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
Sleep we not, therefore, as the rest; but be wakeful and sober.
7 Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
For they who sleep, in the night sleep; and they who are drunken, in the night are drunken.
8 Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
But we who are sons of the day must be wakeful in our minds, and wear the mail-coat of faith and of love, and put on the helmet of the hope of salvation.
9 Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
For Aloha hath not appointed us to wrath, but to the possession of salvation in our Lord Jeshu Meshiha,
10 Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye.
who died on our behalf, that, whether we wake or sleep, together with him we may live.
11 Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.
Wherefore comfort one another, and edify one another, as also you do.
12 Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
BUT I entreat of you, my brethren, to know them who labour among you, and stand before your faces teaching you,
13 Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
that they be esteemed by you in abundant love; and on account of their work be at peace with them.
14 Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
And I entreat of you, my brethren, (to) admonish the offenders, and encourage the little of soul, and bear the burden of the weak, and prolong your spirit toward every man.
15 Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
And beware, lest any of you evil render for evil; but always follow after (those things which are) good (pl.) toward one another, and toward every man.
16 Furahini siku zote;
Be joyful always,
17 ombeni bila kukoma;
and pray without ceasing,
18 shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
and in every thing give thanks; for this is the will of Aloha in Jeshu Meshiha concerning you.
19 Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
The Spirit quench not.
20 msiyadharau maneno ya unabii.
Prophecy do not despise.
21 Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
Prove every thing, and what is good retain.
22 Jiepusheni na uovu wa kila namna.
And from every evil thing flee.
23 Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo.
But the God of peace himself will sanctify perfectly all of you; and your whole spirit, and your soul, and your body will he keep without fault, to the coming of our Lord Jeshu Meshiha.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.
Faithful is he who hath called you, who himself will do it!
25 Ndugu, tuombeeni.
My brethren, pray for us.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Ask the peace of all our brethren, with the holy kiss.
27 Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.
I adjure you, by our Lord, that this epistle be read to all the holy brethren.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.
The grace of our Lord Jeshu Meshiha be with you. Amen.

< 1 Wathesalonike 5 >