< 1 Wathesalonike 5 >

1 Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
Men om Tid og Time, Brødre! have I ikke nødig, at der skrives til eder;
2 kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
thi I vide selv grant, at Herrens Dag kommer som en Tyv om Natten.
3 Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
Naar de sige: „Fred og ingen Fare!” da kommer Undergang pludselig over dem ligesom Veerne over den frugtsommelige, og de skulle ingenlunde undfly.
4 Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
Men I, Brødre! I ere ikke i Mørke, saa at Dagen skulde overraske eder som en Tyv.
5 Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
Thi I ere alle Lysets Børn og Dagens Børn, vi ere ikke Nattens eller Mørkets Børn.
6 Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
Saa lader os da ikke sove ligesom de andre, men lader os vaage og være ædrue!
7 Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
Thi de, som sove, sove om Natten, og de, som beruse sig, ere berusede om Natten.
8 Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
Men da vi høre Dagen til, saa lader os være ædrue, iførte Troens og Kærlighedens Panser og Frelsens Haab som Hjelm!
9 Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Thi Gud bestemte os ikke til Vrede, men til at vinde Frelse ved vor Herre Jesus Kristus,
10 Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye.
som døde for os, for at vi, hvad enten vi vaage eller sove, skulle leve sammen med ham.
11 Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.
Formaner derfor hverandre og opbygger den ene den anden, ligesom I ogsaa gøre.
12 Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
Men vi bede eder, Brødre! at I skønne paa dem, som arbejde iblandt eder og ere eders Forstandere i Herren og paaminde eder.
13 Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
og agte dem højlig i Kærlighed for deres Gernings Skyld. Holder Fred med hverandre!
14 Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
Og vi formane eder, Brødre! paaminder de uskikkelige, trøster de modfaldne, tager eder af de skrøbelige, værer langmodige imod alle!
15 Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
Ser til, at ingen gengælder nogen ondt med ondt; men stræber altid efter det gode, baade imod hverandre og imod alle.
16 Furahini siku zote;
Værer altid glade,
17 ombeni bila kukoma;
beder uafladelig,
18 shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
takker i alle Forhold; thi dette er Guds Villie med eder i Kristus Jesus.
19 Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
Udslukker ikke Aanden,
20 msiyadharau maneno ya unabii.
ringeagter ikke Profetier,
21 Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
prøver alt, beholder det gode!
22 Jiepusheni na uovu wa kila namna.
Holder eder fra det onde under alle Skikkelser!
23 Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo.
Men han selv, Fredens Gud, helliggøre eder ganske og aldeles, og gid eders Aand og Sjæl og Legeme maa bevares helt og holdent, uden Dadel i vor Herres Jesu Kristi Tilkommelse!
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.
Trofast er han, som kaldte eder, han skal ogsaa gøre det.
25 Ndugu, tuombeeni.
Brødre! beder for os!
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Hilser alle Brødrene med et helligt Kys!
27 Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.
Jeg besværger eder ved Herren, at dette Brev maa blive oplæst for alle de hellige Brødre.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.
Vor Herres Jesu Kristi Naade være med eder!

< 1 Wathesalonike 5 >