< 1 Wathesalonike 4 >

1 Hatimaye, ndugu, tuliwaomba na kuwasihi katika Bwana Yesu kwamba, kama mlivyojifunza kutoka kwetu jinsi iwapasavyo kuishi ili kumpendeza Mungu, kama vile mnavyoishi, imewapasa mzidi sana kufanya hivyo.
Finally then, brothers, we implore you and we exhort [you] in [the] Lord Jesus (so that *NO*) even as you have received from us in what manner it behooves you to walk and to please God (even as also you walk [now], *NO*) so you may abound more;
2 Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa mamlaka ya Bwana Yesu.
You know for what instructions we gave you through the Lord Jesus.
3 Mapenzi ya Mungu ni kwamba ninyi mtakaswe, ili kwamba mjiepushe na zinaa,
This for is [the] will of God, the sanctification of you: To abstain you [are] from sexual immorality;
4 ili kwamba kila mmoja wenu ajifunze kuutawala mwili wake mwenyewe katika utakatifu na heshima,
to know each of you [how] the his own vessel to control in holiness and honor,
5 si kwa tamaa mbaya kama watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
not in [the] passion of lust as also the Gentiles not knowing God;
6 Katika jambo hili mtu asimkosee ndugu yake wala kumlaghai. Kwa kuwa Bwana ni mlipiza kisasi katika mambo haya yote, kama vile tulivyokwisha kuwaambia mapema na kuwaonya vikali.
not to go beyond and to overreach in the matter the brother of him; because avenging [is] (the *k*) Lord concerning all these things even as also we told before you and thoroughly warned.
7 Kwa maana Mungu hakutuitia uchafu, bali utakatifu.
Not for has called us God to impurity but into holiness.
8 Kwa hiyo, mtu yeyote anayekataa mafundisho haya hamkatai mwanadamu, bali anamkataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.
So then the [one] rejecting [this] not man disregards but God the [One] also (giving *N(k)O*) the Spirit of Him Holy to (you. *N(K)O*)
9 Sasa kuhusu upendo wa ndugu hamna haja mtu yeyote kuwaandikia, kwa maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana.
Concerning now brotherly love no need you have [for me] to write to you; yourselves for you yourselves taught by God are in order to love one another;
10 Nanyi kwa kweli mnawapenda ndugu wote katika Makedonia nzima. Lakini ndugu, tunawasihi mzidi sana kuwapenda.
And for you are doing this toward all the brothers the [ones] in all Macedonia. We exhort however you, brothers, to abound more and more
11 Jitahidini kuishi maisha ya utulivu, kila mtu akijishughulisha na mambo yake mwenyewe na kufanya kazi kwa mikono yake, kama vile tulivyowaagiza,
and to strive earnestly to live quietly and to attend to [your] own and to work with the own hands of you even as you we commanded;
12 ili maisha yenu ya kila siku yajipatie heshima kutoka kwa watu walio nje, ili msimtegemee mtu yeyote.
so that you may walk properly toward those outside and of no one need may have.
13 Lakini ndugu, hatutaki mkose kujua kuhusu wale waliolala mauti, ili msihuzunike kama watu wengine wasiokuwa na tumaini.
Not (we do want *N(K)O*) but you to be ignorant, brothers, concerning those (themselves falling asleep, *N(k)O*) so that not you may be grieved even as also the rest those not having hope.
14 Kwa kuwa tunaamini kwamba Yesu alikufa na kufufuka, na kwa hivyo, Mungu kwa njia ya Yesu atawafufua pamoja naye wale waliolala mautini ndani yake.
If for we believe that Jesus died and rose again, so also God those having fallen asleep through Jesus will bring with Him.
15 Kulingana na neno la Bwana mwenyewe, tunawaambia kwamba sisi ambao bado tuko hai, tuliobaki hadi kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia waliolala mauti.
This for to you we declare in [the] word of [the] Lord that we ourselves the living who are remaining untill the coming of the Lord certainly not may precede those having fallen asleep;
16 Kwa maana Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni, akitoa amri kwa sauti kuu, pamoja na sauti ya malaika mkuu, na sauti ya tarumbeta ya Mungu. Nao waliokufa wakiwa katika Kristo watafufuka kwanza.
because Himself the Lord with a loud command, with [the] voice of an archangel and with [the] trumpet of God will descend from heaven, and the dead in Christ will rise first,
17 Baada ya hilo sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu ili kumlaki Bwana hewani, hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
Then we ourselves the living those remaining together with them we will be caught away in [the] clouds for [the] meeting of the Lord in [the] air; and so always with [the] Lord we will be.
18 Kwa hiyo farijianeni kwa maneno haya.
Therefore do encourage one another with words these.

< 1 Wathesalonike 4 >