< 1 Wathesalonike 3 >
1 Kwa hivyo tulipokuwa hatuwezi kuvumilia zaidi, tuliamua tubaki Athene peke yetu.
Wherefore being able to contain no longer, we were content to be left alone at Athens,
2 Tukamtuma Timotheo ambaye ni ndugu yetu na mtumishi mwenzetu wa Mungu katika kuieneza Injili ya Kristo, aje kuwaimarisha na kuwatia moyo katika imani yenu,
and sent Timothy our brother, and a minister of God, and our fellow-labourer in the gospel of Christ, to establish and exhort you concerning your faith;
3 ili mtu yeyote asifadhaishwe na mateso haya. Mnajua vyema kwamba tumewekewa hayo mateso.
that no one might be shaken by these afflictions: for ye yourselves know that we are appointed hereunto.
4 Kwa kweli, tulipokuwa pamoja nanyi tuliwaambia mara kwa mara kwamba tutateswa na imekuwa hivyo kama mjuavyo.
For when we were with you, we told you before that we should be afflicted, as it came to pass, and ye know.
5 Kwa sababu hii nilipokuwa siwezi kuvumilia zaidi, nilimtuma mtu ili nipate habari za imani yenu. Niliogopa kwamba kwa njia fulani yule mjaribu asiwe amewajaribu, nasi tukawa tumejitaabisha bure.
For this cause being able to wait no longer, I sent to know the state of your faith, least the tempter should have tempted you, and our labor have been in vain.
6 Lakini sasa Timotheo ndiyo tu amerejea kwetu kutoka kwenu na ameleta habari njema kuhusu imani yenu na upendo wenu. Ametuambia kwamba siku zote mnatukumbuka kwa wema na kwamba mna shauku ya kutuona kama vile sisi tulivyo na shauku ya kuwaona ninyi.
But now Timothy being come back to us from you, and having brought us good tidings concerning your faith and love, and that ye have always a good remembrance of us, greatly desiring to see us, as we indeed do to see you;
7 Kwa hiyo, ndugu zetu, katika dhiki na mateso yetu yote tumefarijika kwa sababu ya imani yenu.
by this we were comforted in you, my brethren, under all our affliction and distress, because of your faith:
8 Sasa kwa kuwa hakika tunaishi, kwa kuwa ninyi mmesimama imara katika Bwana.
for now we are revived, since you are stedfast in the Lord.
9 Je, tutawezaje kumshukuru Mungu kiasi cha kutosha kwa ajili yenu, kutokana na furaha tuliyo nayo mbele za Mungu wetu kwa sababu yenu?
For what thanks can we render to God concerning you, for all the joy wherewith we rejoice on your account before our God,
10 Usiku na mchana tunaomba kwa bidii ili tupate kuwaona tena na kujaza kile kilichopungua katika imani yenu.
night and day most ardently praying, that we may see your face, and perfect whatever is wanting in your faith?
11 Basi Mungu wetu na Baba yetu mwenyewe na Bwana wetu Yesu atengeneze njia ya sisi kuja kwenu.
And may God himself even our Father, and our Lord Jesus Christ direct our way to you:
12 Bwana na auongeze upendo wenu na kuuzidisha kati yenu na kwa wengine wote, kama vile tulivyo na upendo mwingi kwenu.
and the Lord make you to increase and abound in love to one another, and to all men, as we do towards you:
13 Tunamwomba Mungu aimarishe mioyo yenu ili msiwe na lawama katika utakatifu mbele za Mungu wetu aliye Baba yetu wakati wa kuja kwake Bwana Yesu pamoja na watakatifu wote.
that your hearts may be established unblameable in holiness, before God even our Father, at the coming of our Lord Jesus Christ, with all his saints.