< 1 Wathesalonike 3 >

1 Kwa hivyo tulipokuwa hatuwezi kuvumilia zaidi, tuliamua tubaki Athene peke yetu.
我们再也忍受不下去了,于是我们决定留在雅典、
2 Tukamtuma Timotheo ambaye ni ndugu yetu na mtumishi mwenzetu wa Mungu katika kuieneza Injili ya Kristo, aje kuwaimarisha na kuwatia moyo katika imani yenu,
派我们的兄弟提摩太去,这对我们最好了。在传递耶稣福音时,他是我们的兄弟,与上帝一起工作。我们把他派过去,是为了让你们更坚定地相信上帝,给你们勇气,
3 ili mtu yeyote asifadhaishwe na mateso haya. Mnajua vyema kwamba tumewekewa hayo mateso.
让你们任何人都不会因困难而沮丧。你们应该知道,这困难是预料之中的。
4 Kwa kweli, tulipokuwa pamoja nanyi tuliwaambia mara kwa mara kwamba tutateswa na imekuwa hivyo kama mjuavyo.
即使与你们在一起的时候,我们就一直在警告,我们将会遭受困难。你们也知道,事实的确如此。
5 Kwa sababu hii nilipokuwa siwezi kuvumilia zaidi, nilimtuma mtu ili nipate habari za imani yenu. Niliogopa kwamba kwa njia fulani yule mjaribu asiwe amewajaribu, nasi tukawa tumejitaabisha bure.
这就是为什么当我无法在忍受时,就派人去看看你们是否仍然信上帝。我担心魔鬼成功地诱惑了你们,导致我们的努力都白费了!
6 Lakini sasa Timotheo ndiyo tu amerejea kwetu kutoka kwenu na ameleta habari njema kuhusu imani yenu na upendo wenu. Ametuambia kwamba siku zote mnatukumbuka kwa wema na kwamba mna shauku ya kutuona kama vile sisi tulivyo na shauku ya kuwaona ninyi.
造访你们的提摩太刚刚返回,带给你们对上帝的信和你们的爱告诉我们,这是一个好消息。他还告诉我们,你们仍然会想起我们,希望见到我们,就像我们想见你们一样。
7 Kwa hiyo, ndugu zetu, katika dhiki na mateso yetu yote tumefarijika kwa sababu ya imani yenu.
兄弟姐妹们,当我们在经历苦痛时,得知你们仍然坚持对上帝的信,这消息真正地鼓励了我们。
8 Sasa kwa kuwa hakika tunaishi, kwa kuwa ninyi mmesimama imara katika Bwana.
因为你们坚定地与主站在一起,对我们而言就值得继续活下去。
9 Je, tutawezaje kumshukuru Mungu kiasi cha kutosha kwa ajili yenu, kutokana na furaha tuliyo nayo mbele za Mungu wetu kwa sababu yenu?
你们给我们带来了快乐,当我们来到上帝面前,我们怎么能不为此感谢上帝呢?
10 Usiku na mchana tunaomba kwa bidii ili tupate kuwaona tena na kujaza kile kilichopungua katika imani yenu.
我们热切地日夜祈求,希望能再次与你们见面,帮助你们继续培养对上帝的信。
11 Basi Mungu wetu na Baba yetu mwenyewe na Bwana wetu Yesu atengeneze njia ya sisi kuja kwenu.
愿我们的父上帝和我们的主耶稣,能让我们可以尽快到你们那里去。
12 Bwana na auongeze upendo wenu na kuuzidisha kati yenu na kwa wengine wote, kama vile tulivyo na upendo mwingi kwenu.
愿主增加你们的爱,让这爱可以溢出并彼此流淌,流淌到每个人那里,就像我们爱你们一样。
13 Tunamwomba Mungu aimarishe mioyo yenu ili msiwe na lawama katika utakatifu mbele za Mungu wetu aliye Baba yetu wakati wa kuja kwake Bwana Yesu pamoja na watakatifu wote.
通过这种方式,愿耶稣让你们坚定。在我们主耶稣和众圣徒到来的时候,你们能站在我们的父上帝面前,完全圣洁,无可指责。

< 1 Wathesalonike 3 >