< 1 Wathesalonike 2 >

1 Ndugu zangu, kwa kuwa ninyi wenyewe mnajua ya kwamba kuja kwetu kwenu hakukuwa bure,
Te teate hästi, vennad ja õed, et meie külaskäik teie juurde ei olnud tulemusteta.
2 kama vile mjuavyo, tulikuwa tumeteswa na kutukanwa huko Filipi, lakini hata hivyo, kwa msaada wa Mungu wetu, tulikuwa na ujasiri wa kuwaambia Injili ya Mungu ingawa kulikuwa na upinzani mkubwa.
Kuigi, nagu te teate, me olime eelnevalt kannatanud ja meid teotati Filippis, andis Jumal meile siiski julguse kuulutada tema evangeeliumi rohkele vastuseisule vaatamata.
3 Kwa maana himizo letu halikutokana na hila wala nia mbaya au udanganyifu.
Kutse, mille me esitasime, ei ole ajendatud eksitusest või räpasest tagamõttest. Samuti ei püüa me teid kavalusega võita.
4 Kinyume chake, tulinena kama watu tuliokubaliwa na Mungu tukakabidhiwa Injili. Sisi hatujaribu kuwapendeza wanadamu bali kumpendeza Mungu, yeye ayachunguzaye mawazo ya ndani sana ya mioyo yetu.
Vastupidi, me kuulutame kui need, kelle Jumal on heaks kiitnud ja kellele ta on oma evangeeliumi usaldanud. Me ei püüa meeldida inimestele, vaid Jumalale, kes uurib läbi meie südamed.
5 Kama mjuavyo, hatukuja kwenu kwa maneno ya kujipendekeza au maneno yasiyo ya kweli ili kuficha tamaa mbaya: Mungu ndiye shahidi yetu.
Te teate, et me ei ole kunagi tulnud meelitavate sõnade ega varjatud ahnusega: Jumal on meie tunnistajaks.
6 Wala hatukuwa tunatafuta sifa kutoka kwa wanadamu, wala kutoka kwenu au kwa mtu mwingine awaye yote. Kama mitume wa Kristo tungaliweza kuwa mzigo kwenu,
Me ei otsi kiitust inimestelt, ei teilt ega kelleltki teiselt,
7 lakini tulikuwa wapole katikati yenu, kama mama anayewatunza watoto wake wadogo.
ehkki me võiksime Kristuse apostlitena rõhutada oma tähtsust. Selle asemel olime leebed teie keskel. Nii nagu imetav ema kannab hoolt oma laste eest,
8 Tuliwapenda sana kiasi kwamba tulifurahia kushirikiana nanyi, si Injili ya Mungu tu, bali hata maisha yetu, kwa sababu mlikuwa wa thamani mno kwetu.
nii hoolitsesime meiegi teie eest. Kuna me armastasime teid nii väga, oli meil hea meel jagada teiega mitte ainult Jumala evangeeliumi, vaid ka meie elu.
9 Ndugu zetu, mnakumbuka juhudi yetu na taabu yetu. Tulifanya kazi usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote wa kwenu wakati tulipokuwa tunawahubiria Injili ya Mungu.
Te ju mäletate, vennad ja õed, meie vaeva ja raskusi! Me töötasime ööd ja päevad, et teid mitte koormata samal ajal, kui me Jumala evangeeliumi kuulutasime.
10 Ninyi wenyewe ni mashahidi na Mungu pia, jinsi tulivyokuwa watakatifu, wenye haki na wasio na lawama miongoni mwenu ninyi mlioamini.
Teie ise koos Jumalaga olete tunnistajaks, kui pühad, õiglased ja laitmatud me olime usklike hulgas.
11 Maana mnajua kwamba tuliwatendea kila mmoja wenu kama vile baba awatendeavyo watoto wake.
Sest te teate, et me käitusime igaühega teie hulgast nii, nagu isa käitub omaenda lastega,
12 Tuliwatia moyo, tuliwafariji na kuwahimiza kuishi maisha yampendezayo Mungu, anayewaita katika Ufalme na utukufu wake.
julgustades, lohutades ja innustades teid elama Jumala vääriliselt, kes teid kutsub oma Kuningriiki ja kirkusse.
13 Nasi pia tunamshukuru Mungu bila kukoma kwa sababu mlipolipokea neno la Mungu mlilosikia kutoka kwetu, hamkulipokea kama neno la wanadamu, bali mlilipokea kama lilivyo hasa, neno la Mungu, litendalo kazi ndani yenu ninyi mnaoamini.
Ja seepärast me täname alatasa Jumalat, et kui te meie käest kuulsite Jumala sõna, ei võtnud te seda vastu inimliku sõnana, vaid sellena, mis see tõesti on, Jumala sõnana, mis tegutseb ka teis, kes te usute.
14 Kwa maana ninyi ndugu zetu, mlifanyika wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyoko ndani ya Kristo Yesu katika Uyahudi. Mlipata mateso yale yale kutoka kwa watu wenu wenyewe kama vile makanisa hayo yalivyoteswa na Wayahudi,
Sest teie, vennad ja õed, olete saanud sarnaseks nende Jumala kogudustega Juudamaal, mis on Jeesuses Kristuses: sest ka teie olete saanud kannatada oma inimeste poolt, nii nagu need kogudused juutide poolt.
15 wale waliomuua Bwana Yesu na manabii, nasi wakatufukuza pia. Watu hao walimchukiza Mungu na tena ni adui wa watu wote,
Nad tapsid ka Issanda Jeesuse ning prohvetid ja ajasid ka meid minema. Nad ei ole Jumalale meelepärased ja on vaenulikud kõigi inimeste vastu,
16 wakijitahidi kutuzuia tusizungumze na watu wa Mataifa ili kwamba wapate kuokolewa. Kwa njia hii wanazidi kujilundikia dhambi zao hadi kikomo. Lakini hatimaye ghadhabu ya Mungu imewafikia.
takistades meid kõnelemast rahvastele nende päästmiseks. Nii täidavad nad igati oma pattude mõõtu. Ent Jumala viha on tulnud nende peale täie jõuga.
17 Lakini ndugu zetu, tulipotenganishwa nanyi kwa kitambo kidogo (ingawa kutengana huko kulikuwa kwa mwili tu, si kwa moyo), tulizidi kuwa na shauku kubwa kuwaona uso kwa uso.
Meie aga, vennad ja õed, olles küll lühikeseks ajaks teist eraldatud (ihulikult, mitte aga südameis), oleme sügavas igatsuses teinud kõik, et teid jälle näha.
18 Maana tulitaka kuja kwenu, hasa mimi Paulo, nilitaka kuja tena na tena, lakini Shetani akatuzuia.
Me oleme tahtnud tulla teie juurde – vähemalt mina, Paulus, ikka ja jälle –, aga saatan on meid takistanud.
19 Kwa maana tumaini letu ni nini, au furaha yetu au taji yetu ya kujisifia mbele za Bwana Yesu Kristo wakati wa kuja kwake? Je, si ni ninyi?
Sest kes siis veel, kui mitte teie, olete meie lootus, meie rõõm ja meie võidupärg Issanda Jeesuse ees tema tagasitulekul?
20 Naam, ninyi ndio fahari yetu na furaha yetu.
Teie olete meie kirkus ja rõõm!

< 1 Wathesalonike 2 >